Obadia Utangulizi
Utangulizi
Maana ya jina Obadia ni “Mtumishi wa Yehova.” Hakuna habari zinazojulikana kuhusu huyu nabii isipokuwa mambo yaliyoandikwa katika kitabu hiki. Obadia alitoa unabii kuhusu hukumu ya Mungu dhidi ya taifa la Edomu, kukomeshwa na kuangamizwa kwalo lisiwepo tena ulimwenguni. Waedomu, waliokuwa uzao wa Esau, walijivunia usalama katika ngome zao zilizokuwa Mlima Seiri, kusini mwa Bahari ya Chumvi. Waliwatazama watu wa Yuda walipopatwa na mikasa mikononi mwa wavamizi bila kuwasaidia. Mwanzoni mwa karne ya tisa Waedomu wenyewe walishiriki zaidi ya mara nne kuiteka nyara Yerusalemu.
Mwandishi
Obadia.
Kusudi
Kuonyesha kwamba Mungu anawahukumu wale wanaowadhuru watu wake.
Mahali
Yerusalemu.
Tarehe
Kati ya 605–586 K.K.
Wahusika Wakuu
Waedomu.
Wazo Kuu
Obadia alitangaza hukumu ya Mungu dhidi ya Waedomu, na akatabiri kuangamizwa kwao na kufutwa kwa kumbukumbu lao katika uso wa dunia. Wale wanaopigana na watu walioitwa na Mungu, yeye hupigana nao na kufuta kumbukumbu lao duniani wasipotubu.
Mambo Muhimu
Hukumu ya Mungu, na kuangamizwa kwa taifa la Waedomu.
Mgawanyo
Maangamizi ya Edomu (1-14)
Kurejezwa kwa Israeli (15-21).
Iliyochaguliwa sasa
Obadia Utangulizi: NEN
Kuonyesha
Shirikisha
Nakili
Je, ungependa vivutio vyako vihifadhiwe kwenye vifaa vyako vyote? Jisajili au ingia
Neno: Biblia Takatifu™ Neno™
Hakimiliki © 1984, 1989, 2009, 2015 na Biblica, Inc.
Imetumiwa kwa ruhusa. Haki zote zimehifadhiwa duniani kote.
Kiswahili Contemporary Version™
Copyright © 1984, 1989, 2009, 2015 by Biblica, Inc.
Used with Permission. All Rights Reserved Worldwide.