Zaburi 129
129
Zaburi 129
Maombi dhidi ya adui za Israeli
Wimbo wa kwenda juu.
1Wamenitesa sana tangu ujana wangu;
Israeli na aseme sasa:
2wamenitesa sana tangu ujana wangu,
lakini bado hawajanishinda.
3Wakulima wamelima mgongo wangu,
na kufanya mifereji yao mirefu.
4Lakini Mwenyezi Mungu ni mwenye haki;
amenifungua toka kamba za waovu.
5Wale wote wanaoichukia Sayuni
na warudishwe nyuma kwa aibu.
6Wawe kama majani juu ya paa,
ambayo hunyauka kabla hayajakua;
7kwa hayo mvunaji hawezi kujaza vitanga vyake,
wala akusanyaye kujaza mikono yake.
8Wale wapitao karibu na wasiseme,
“Baraka ya Mwenyezi Mungu iwe juu yako;
tunakubariki katika jina la Mwenyezi Mungu.”
Iliyochaguliwa sasa
Zaburi 129: NENO
Kuonyesha
Shirikisha
Nakili

Je, ungependa vivutio vyako vihifadhiwe kwenye vifaa vyako vyote? Jisajili au ingia
Neno: Maandiko Matakatifu™ NMM™
Hakimiliki © 2018, 2024 na Biblica, Inc.
Imetumiwa kwa ruhusa.
Haki zote zimehifadhiwa duniani kote.
Kiswahili Contemporary Scriptures™
Copyright © 2018, 2024 by Biblica, Inc.
Used with permission. All rights reserved worldwide.