Chapa ya Youversion
Ikoni ya Utafutaji

Zaburi 14

14
Zaburi 14
Uovu wa wanadamu
(Zaburi 53)
Kwa mwimbishaji. Zaburi ya Daudi.
1Mpumbavu anasema moyoni mwake,
“Hakuna Mungu.”
Wamepotoka, matendo yao ni maovu kabisa;
hakuna hata mmoja atendaye mema.
2Mwenyezi Mungu anawachungulia wanadamu
kutoka mbinguni
aone kama kuna mwenye hekima,
yeyote anayemtafuta Mungu.
3Wote wamepotoka,
wote wameoza pamoja;
hakuna atendaye mema,
naam, hakuna hata mmoja!
4Je, watendao maovu kamwe hawatajifunza:
wale ambao huwala watu wangu
kama watu walavyo mkate,
hao ambao hawamwiti Mwenyezi Mungu?
5Wako hapo, wameingiwa na hofu kuu,
maana Mungu yupo pamoja na wenye haki.
6Ninyi watenda maovu mnakwamisha mipango ya maskini,
bali Mwenyezi Mungu ndiye kimbilio lao.
7Laiti wokovu wa Israeli
ungekuja kutoka Sayuni!
Mwenyezi Mungu anaporejesha
wafungwa wa watu wake,
Yakobo na ashangilie,
Israeli na afurahi!

Iliyochaguliwa sasa

Zaburi 14: NENO

Kuonyesha

Shirikisha

Nakili

None

Je, ungependa vivutio vyako vihifadhiwe kwenye vifaa vyako vyote? Jisajili au ingia