Chapa ya Youversion
Ikoni ya Utafutaji

Zaburi 43

43
Zaburi 43#43:0 Katika nakala za kale za Kiebrania, Zaburi 42 na 43 ni moja
Maombi ya mtu aliye uhamishoni yanaendelea
1Ee Mungu unihukumu,
nitetee dhidi ya taifa lisilomcha Mungu,
niokoe na watu wadanganyifu na waovu.
2Wewe ni Mungu ngome yangu.
Kwa nini umenikataa?
Kwa nini niendelee kuomboleza,
nikidhulumiwa na adui?
3Tuma hima nuru yako na kweli yako viniongoze;
na vinilete hadi mlima wako mtakatifu,
mahali unapoishi.
4Ndipo nitaenda madhabahuni pa Mungu,
kwa Mungu, furaha yangu na shangwe yangu.
Nitakusifu kwa kinubi,
Ee Mungu, Mungu wangu.
5Ee nafsi yangu, kwa nini unasononeka?
Kwa nini unafadhaika hivyo ndani yangu?
Weka tumaini lako kwa Mungu,
kwa sababu bado nitamsifu
Mwokozi wangu na Mungu wangu.

Iliyochaguliwa sasa

Zaburi 43: NENO

Kuonyesha

Shirikisha

Nakili

None

Je, ungependa vivutio vyako vihifadhiwe kwenye vifaa vyako vyote? Jisajili au ingia