Chapa ya Youversion
Ikoni ya Utafutaji

Zaburi 65

65
Zaburi 65
Kusifu na kushukuru
Kwa mwimbishaji. Zaburi ya Daudi. Wimbo.
1Ee Mungu, sifa zakungojea katika Sayuni;
kwako wewe nadhiri zetu zitatimizwa.
2Ewe usikiaye maombi,
watu wote watakuja kwako wewe.
3Tulipokuwa tumefunikwa kabisa na dhambi,
wewe ulisamehe makosa yetu.
4Heri wale uliowachagua
na kuwaleta karibu ili waishi katika nyua zako!
Tunashibishwa kwa mema ya nyumba yako,
mema ya Hekalu lako takatifu.
5Unatujibu kwa matendo ya kushangaza ya haki,
Ee Mungu Mwokozi wetu,
tumaini la miisho yote ya duniani
na la bahari zilizo mbali sana,
6uliyeumba milima kwa uwezo wako,
ukiwa umejivika nguvu,
7uliyenyamazisha dhoruba za bahari,
ngurumo za mawimbi yake,
na ghasia za mataifa.
8Wale wanaoishi mbali sana
wanaogopa maajabu yako,
kule asubuhi ipambazukiapo
na kule jioni inakofifilia
umeziita nyimbo za furaha.
9Waitunza nchi na kuinyeshea,
waitajirisha kwa wingi.
Vijito vya Mungu vimejaa maji
ili kuwapa watu nafaka,
kwa maana wewe umeviamuru.
10Umeilowesha mifereji yake
na kusawazisha kingo zake;
umeilainisha kwa manyunyu
na kuibariki mimea yake.
11Umeuvika mwaka taji la baraka,
magari yako yanafurika kwa wingi.
12Mbuga za majani za jangwani umezineemesha;
vilima vimevikwa furaha.
13Malisho yamejaa makundi ya wanyama,
na mabonde yamepambwa kwa mavuno;
vyote vinashangilia kwa furaha na kuimba.

Iliyochaguliwa sasa

Zaburi 65: NENO

Kuonyesha

Shirikisha

Nakili

None

Je, ungependa vivutio vyako vihifadhiwe kwenye vifaa vyako vyote? Jisajili au ingia