Zab 13
13
Sala ya Ukombozi kutoka kwa Adui
Kwa mwimbishaji. Zaburi ya Daudi.
1 #
Kum 31:17; Ayu 13:24; Zab 22:1; Isa 59:2 Ee BWANA, hata lini utanisahau, hata milele?
Hata lini utanificha uso wako?
2Hata lini nifanye mashauri nafsini mwangu,
Nikihuzunika moyoni mchana kutwa?
Hata lini adui yangu atukuke juu yangu?
3 #
Ezr 9:8; Zab 18:28; Lk 2:32; Ufu 21:23; Zab 76:5,6; Isa 37:36; Yer 51:39; Efe 5:14 Ee BWANA, Mungu wangu, uangalie, uniitikie;
Uyatie nuru macho yangu,
Nisije nikalala usingizi wa mauti.
4Adui yangu asije akasema, Nimemshinda;
Watesi wangu wasifurahi ninapoondoshwa.
5 #
2 Nya 20:12
Nami nimezitumainia fadhili zako;
Moyo wangu na uufurahie wokovu wako.
6Naam, nimwimbie BWANA,
Kwa kuwa amenitendea kwa ukarimu.
Iliyochaguliwa sasa
Zab 13: SUV
Kuonyesha
Shirikisha
Nakili
![None](/_next/image?url=https%3A%2F%2Fimageproxy.youversionapistaging.com%2F58%2Fhttps%3A%2F%2Fweb-assets.youversion.com%2Fapp-icons%2Fsw.png&w=128&q=75)
Je, ungependa vivutio vyako vihifadhiwe kwenye vifaa vyako vyote? Jisajili au ingia
Swahili Union Version (SUV): © Bible Society of Tanzania and Bible Society of Kenya, 1952, 1997. All rights reserved. lt/pgt ltpgtSwahili Union Version (SUV): Hakimiliki -1952, 1997: kwa: Chama cha Biblia cha Tanzania na Chama cha Biblia cha Kenya. Haki zote zimehifadhiwa.