Zab 15
15
Nani Atakaa katika Patakatifu pa Mungu?
Zaburi ya Daudi.
1 #
Zab 2:5
BWANA, ni nani atakayekaa
Katika hema yako?
Ni nani atakayefanya maskani yake
Katika kilima chako kitakatifu?
2 #
Zab 84:11; Isa 33:15,16 Ni mtu aendaye kwa ukamilifu,
Na kutenda haki.
Asemaye kweli kwa moyo wake,
3Asiyesingizia kwa ulimi wake.
Wala hakumtenda mwenziwe mabaya,
Wala hakumsengenya jirani yake.
4 #
Yos 9:18-20
Machoni pake mtu asiyefaa hudharauliwa,
Bali huwaheshimu wamchao BWANA
Ingawa ameapa kwa hasara yake,
Hayabadili maneno yake.
5 #
Eze 18:8,9 Hakutoa fedha yake apate kula riba,
Hakutwaa rushwa amwangamize asiye na hatia.
Mtu atendaye mambo hayo
Hataondoshwa milele.
Iliyochaguliwa sasa
Zab 15: SUV
Kuonyesha
Shirikisha
Nakili
![None](/_next/image?url=https%3A%2F%2Fimageproxy.youversionapistaging.com%2F58%2Fhttps%3A%2F%2Fweb-assets.youversion.com%2Fapp-icons%2Fsw.png&w=128&q=75)
Je, ungependa vivutio vyako vihifadhiwe kwenye vifaa vyako vyote? Jisajili au ingia
Swahili Union Version (SUV): © Bible Society of Tanzania and Bible Society of Kenya, 1952, 1997. All rights reserved. lt/pgt ltpgtSwahili Union Version (SUV): Hakimiliki -1952, 1997: kwa: Chama cha Biblia cha Tanzania na Chama cha Biblia cha Kenya. Haki zote zimehifadhiwa.