Chapa ya Youversion
Ikoni ya Utafutaji

Zab 82

82
Ombi la Kupata Haki
Zaburi ya Asafu.
1 # Mhu 5:8; Kut 21:6 Mungu asimama katika kusanyiko la Mungu;
Katikati ya miungu anahukumu.
2 # Kum 1:17; Zab 58:1,2 Hata lini mtahukumu kwa dhuluma,
Na kuzikubali nyuso za wabaya?
3Mfanyieni hukumu maskini na yatima;
Mtendeeni haki aliyeonewa na fukara;
4Mwokoeni maskini na mhitaji;
Mwopoeni mikononi mwa wadhalimu.
5 # Zab 11:3 Hawajui wala hawafahamu, hutembea gizani;
Misingi yote ya nchi imetikisika.
6 # Ayu 21:32; Eze 31:14; Yn 10:34 Mimi nimesema, Ndinyi miungu,
Na wana wa Aliye juu, nyote pia.
7Lakini mtakufa kama wanadamu,
Mtaanguka kama mmoja wa wakuu.
8 # Zab 2:8; Ufu 11:15 Ee Mungu, usimame, uihukumu nchi,
Maana Wewe utawarithi mataifa yote.

Iliyochaguliwa sasa

Zab 82: SUV

Kuonyesha

Shirikisha

Nakili

None

Je, ungependa vivutio vyako vihifadhiwe kwenye vifaa vyako vyote? Jisajili au ingia