Chapa ya Youversion
Ikoni ya Utafutaji

Zab 89:38-52

Zab 89:38-52 SUV

Walakini Wewe umemtupa na kumkataa, Umemghadhibikia masihi wako. Umechukizwa na agano la mtumishi wako, Umeinajisi taji yake na kuitupa chini. Umeyabomoa maboma yake yote, Umezifanya ngome zake kuwa magofu. Wote wapitao njiani wanateka mali zake; Amekuwa laumu kwa jirani zake; Umeutukuza mkono wa kuume wa watesi wake; Umewafurahisha wote wanaomchukia. Pia umeurudisha nyuma ukali wa upanga wake; Wala hukumsimamisha vitani. Umeikomesha fahari yake; Kiti chake cha enzi umekitupa chini. Umezipunguza siku za ujana wake; Umemvika aibu. Ee BWANA, hata lini? Utajificha hata milele? Ghadhabu yako itawaka kama moto? Ukumbuke jinsi mimi nisivyo wa kudumu; Kwa ubatili gani umeiumba jamii ya wanadamu! Ni mwanamume gani atakayeishi asione mauti, Atakayejiokoa nafsi yake na mkono wa kuzimu? Bwana, zi wapi fadhili zako za kwanza, Ulizomwapia Daudi kwa uaminifu wako? Ee Bwana, ukumbuke, Wanavyosimangwa watumishi wako; Jinsi ninavyostahimili kifuani mwangu Masimango ya watu wengi. Ambayo adui zako wamesimanga, Ee BWANA, Naam, wamezisimanga hatua za masihi wako. Na ahimidiwe BWANA milele. Amina na Amina.

Mipango ya Kusoma Bila Malipo na Ibada zinazohusiana na Zab 89:38-52