Chapa ya Youversion
Ikoni ya Utafutaji

Zaburi 89:38-52

Zaburi 89:38-52 SRUV

Lakini wewe umemtupa na kumkataa, Umemghadhibikia masihi wako. Umechukizwa na agano la mtumishi wako, Umelinajisi taji lake na kulitupa chini. Umeyabomoa maboma yake yote, Umezifanya ngome zake kuwa magofu. Wote wapitao njiani wanateka mali zake; Amedharauliwa na jirani zake; Umeutukuza mkono wa kulia wa watesi wake; Umewafurahisha wote wanaomchukia. Pia umeurudisha nyuma ukali wa upanga wake; Wala hukumsimamisha vitani. Umeikomesha fahari yake; Kiti chake cha enzi umekitupa chini. Umezipunguza siku za ujana wake; Umemvika aibu. Hadi lini, Ee BWANA? Utajificha hata milele? Ghadhabu yako itawaka kama moto hadi lini? Ukumbuke jinsi mimi nisivyo wa kudumu; Kwa ubatili gani umeiumba jamii ya wanadamu! Ni mwanamume gani atakayeishi asione mauti, Atakayejiokoa nafsi yake na mkono wa kuzimu? Bwana, ziko wapi fadhili zako za kwanza, Ulizomwapia Daudi kwa uaminifu wako? Ukumbuke, Ee Bwana, Wanavyosimangwa watumishi wako; Jinsi ninavyostahimili kifuani mwangu Masimango ya watu wengi. Ambayo adui zako wamesimanga, Ee BWANA, Naam, wamezisimanga hatua za masihi wako. Na ahimidiwe BWANA milele. Amina na Amina.

Soma Zaburi 89

Mipango ya Kusoma Bila Malipo na Ibada zinazohusiana na Zaburi 89:38-52