Zek UTANGULIZI
UTANGULIZI
Katika Biblia kuna watu wapatao thelathini waitwao Zekaria. Wengi wa hao ni viongozi (2 Fal 15:8-11, 14:29), makuhani (2 Nya 24:20-26) na manabii. Kati ya manabii hao, ajulikanaye sana ni Zekaria wa kitabu hiki (1–8). Maana ya jina Zekaria ni “aliyekumbukwa na BWANA”. Zekaria mwandishi wa kitabu hiki ni wa ukoo wa makuhani (Neh 12:4, 16), aliishi Yerusalemu baada ya Wayahudi kutoka uhamishoni. Alianza kutoa ujumbe akiwa bado kijana (2:4) karibu miezi miwili baada ya ujumbe wa Hagai. Zekaria na Hagai walikuwa manabii wenza waliohimiza ujenzi wa Hekalu la Yerusalemu (Ezra 4:1-5, 24; 5:1-2; 6:14-15 tazama pia Utangulizi wa Hagai).
Ujumbe wa Zekaria ni faraja kwa watu waliotoka utumwani Babeli. Vile vile anahimiza uamsho wa kiroho ili wajenge hekalu upya, na kutoa unabii wa matumaini juu ya maisha. Huyu Masihi wa BWANA ataingia Yerusalemu (9:9); atauzwa kwa fedha (11:12-13, 12:10), atakufa kama mchungaji baada ya kupigwa (13:7), atarudi tena kwenye mlima wa mizeituni (14:4) na atatawala miaka elfu akiwa mfalme na kuhani mkuu (14:9).
Yaliyomo:
1. Wito wa kumrudia Mungu, Sura 1:1-6
2. Maono manane ya Zekaria, Sura 1:7–6:8
3. Kutangazwa kwa Yoshua, Sura 6:9-15
4. Suala la kufunga, Sura 7–8
5. Hukumu na ukombozi, Sura 9–13
6. Unabii juu ya Masihi, Sura 14
Iliyochaguliwa sasa
Zek UTANGULIZI: SUV
Kuonyesha
Shirikisha
Nakili
Je, ungependa vivutio vyako vihifadhiwe kwenye vifaa vyako vyote? Jisajili au ingia
Swahili Union Version (SUV): © Bible Society of Tanzania and Bible Society of Kenya, 1952, 1997. All rights reserved. lt/pgt ltpgtSwahili Union Version (SUV): Hakimiliki -1952, 1997: kwa: Chama cha Biblia cha Tanzania na Chama cha Biblia cha Kenya. Haki zote zimehifadhiwa.