Zaburi 137
137
Maombolezo juu ya maangamizi ya Yerusalemu
1 #
Eze 1:1; Dan 8:2; Isa 24:8; Omb 5:15; Amo 8:10; Ufu 18:22 Kando ya mito ya Babeli ndiko tulikoketi,
Tukalia tulipoikumbuka Sayuni.
2Katika miti iliyo katikati yake
Tulivitundika vinubi vyetu.
3Maana huko waliotuchukua mateka
Walitaka tuwaimbie;
Na waliotuonea walitaka tuwatumbuize;
Tuimbieni baadhi ya nyimbo za Sayuni.
4Twawezaje kuimba wimbo wa BWANA
Katika nchi ya ugeni?
5Nikikusahau, Ee Yerusalemu,
Mkono wangu wa kulia na upooze.
6 #
Eze 3:26
Ulimi wangu na ugandamane
Na kaakaa la kinywa changu, nisipokukumbuka.
Nisipoikuza Yerusalemu
Zaidi ya furaha yangu iliyo kuu.
7 #
Omb 4:22; Oba 1:10 Ee BWANA, uwakumbuke wana wa Edomu,
Siku ile Yerusalemu ilipotekwa.
Kwa namna walivyosema, Bomoeni!
Bomoeni hata misingini!
8 #
Isa 13:1; Ufu 18:6 Ee binti Babeli, uliye karibu na kuangamia,
Heri atakayekupatiliza, ulivyotupatiliza sisi.
9Heri yeye atakayewakamata wadogo wako,
Na kuwaseta wao juu ya mwamba.
Iliyochaguliwa sasa
Zaburi 137: SRUV
Kuonyesha
Shirikisha
Nakili
Je, ungependa vivutio vyako vihifadhiwe kwenye vifaa vyako vyote? Jisajili au ingia
Swahili Revised Union Version Bible © Bible Society of Kenya, and Bible Society of Tanzania, 2005.
Zaburi 137
137
Maombolezo juu ya maangamizi ya Yerusalemu
1 #
Eze 1:1; Dan 8:2; Isa 24:8; Omb 5:15; Amo 8:10; Ufu 18:22 Kando ya mito ya Babeli ndiko tulikoketi,
Tukalia tulipoikumbuka Sayuni.
2Katika miti iliyo katikati yake
Tulivitundika vinubi vyetu.
3Maana huko waliotuchukua mateka
Walitaka tuwaimbie;
Na waliotuonea walitaka tuwatumbuize;
Tuimbieni baadhi ya nyimbo za Sayuni.
4Twawezaje kuimba wimbo wa BWANA
Katika nchi ya ugeni?
5Nikikusahau, Ee Yerusalemu,
Mkono wangu wa kulia na upooze.
6 #
Eze 3:26
Ulimi wangu na ugandamane
Na kaakaa la kinywa changu, nisipokukumbuka.
Nisipoikuza Yerusalemu
Zaidi ya furaha yangu iliyo kuu.
7 #
Omb 4:22; Oba 1:10 Ee BWANA, uwakumbuke wana wa Edomu,
Siku ile Yerusalemu ilipotekwa.
Kwa namna walivyosema, Bomoeni!
Bomoeni hata misingini!
8 #
Isa 13:1; Ufu 18:6 Ee binti Babeli, uliye karibu na kuangamia,
Heri atakayekupatiliza, ulivyotupatiliza sisi.
9Heri yeye atakayewakamata wadogo wako,
Na kuwaseta wao juu ya mwamba.
Iliyochaguliwa sasa
:
Kuonyesha
Shirikisha
Nakili
Je, ungependa vivutio vyako vihifadhiwe kwenye vifaa vyako vyote? Jisajili au ingia
Swahili Revised Union Version Bible © Bible Society of Kenya, and Bible Society of Tanzania, 2005.