Chapa ya Youversion
Ikoni ya Utafutaji

Zaburi 53

53
Kushutumiwa kwa wasiomwamini Mungu
Kwa mwimbishaji: kwa mtindo wa Mahalathi. Utenzi wa Daudi.
1 # Rum 3:10-12; Zab 10:4 Mpumbavu husema moyoni, Hakuna Mungu;
Ni wafisadi, na wametenda mambo ya kuchukiza,
Hakuna atendaye mema.
2 # Zab 33:13; 2 Nya 15:2 Toka mbinguni MUNGU aliwachungulia wanadamu,
Aone kama yuko mtu mwenye hekima,
Amtafutaye Mungu.
3 # Mhu 7:29 Kila mtu amepotoka, wameoza wote pamoja,
Hakuna atendaye mema,
La! Hata mmoja.
4 # Yer 4:22 Je! Wafanyao maovu hawajui?
Walao watu wangu kama walavyo mkate,
Hawakumwita MUNGU.
5Hapo waliingiwa na hofu pasipokuwapo hofu,
Maana Mungu ameitawanya mifupa yake aliyekuhusuru.
Umewatia aibu,
Kwa sababu MUNGU amewadharau.
6Laiti wokovu wa Israeli utoke katika Sayuni!
MUNGU awarudishapo wafungwa wa watu wake;
Yakobo atashangilia,
Israeli atafurahi.

Iliyochaguliwa sasa

Zaburi 53: SRUV

Kuonyesha

Shirikisha

Nakili

None

Je, ungependa vivutio vyako vihifadhiwe kwenye vifaa vyako vyote? Jisajili au ingia