Chapa ya Youversion
Ikoni ya Utafutaji

Zaburi 68

68
Sifa na shukrani
Kwa mwimbishaji. Ya Daudi. Zaburi. Wimbo.
1Mungu na ainuke, adui zake watawanyike,
Nao wamchukiao huukimbia uso wake.
2Kama moshi upeperushwavyo,
Ndivyo uwapeperushavyo wao;
Kama nta iyeyukavyo mbele ya moto,
Ndivyo waovu wapoteavyo usoni pa Mungu.
3Bali wenye haki hufurahi,
Na kuushangilia uso wa Mungu,
Naam, hupiga kelele kwa furaha.
4Mwimbieni Mungu, lisifuni jina lake,
Mwimbieni wimbo yeye apitaye katika mawingu,
Jina lake ni YAHU;#68:4 Ufupisho wa YAHWEH.
Shangilieni mbele zake.
5Baba wa yatima na mwamuzi wa wajane,
Ni Mungu aliye katika kao lake takatifu.
6 # 1 Sam 2:5 Mungu huwapa wapweke makao yao;
Huwapa wafungwa uhuru na kuwafanikisha;
Bali wakaidi huishi katika nchi kavu.
7 # Hab 3:13 Ee Mungu, ulipowaongoza watu wako,
Ulipopita nyikani,
8 # Kut 19:18 Nchi ilitetemeka
Naam, mbingu zilidondoka usoni pa Mungu;
Hata Sinai usoni pa Mungu; Mungu wa Israeli.
9Ee Mungu, ulinyesha mvua ya neema;
Urithi wako ulipochoka uliutia nguvu.
10 # Zab 74:19 Watu wako wakafanya makao ya huko;
Ee Mungu, kwa wema wako uliwaruzuku walioonewa.
11Bwana analitoa neno lake;
Wanawake watangazao habari ni jeshi kubwa;
12Wafalme wa majeshi wanakimbia, wanakimbia;
Na mwanamke akaaye nyumbani anagawa nyara.
13 # Zab 81:6; Efe 5:26,27 Kwa nini kulala mazizini arukapo hua,
Mbawa zake ziking'aa kama fedha
Na manyoya yake kama dhahabu?
14Mwenyezi Mungu alipotawanya wafalme huko,
Kulinyesha theluji katika Salmoni.
15Ni mlima wa Mungu mlima Bashani,
Ni mlima mrefu mlima Bashani.
16Enyi milima mirefu, kwani kuutazama kwa wivu
Mlima alioutamani Mungu akae juu yake?
Naam, BWANA atakaa juu yake milele.
17 # Kum 33:2; 2 Fal 6:17; Dan 7:10 Magari ya Mungu ni elfu ishirini, maelfu kwa maelfu;
Bwana yumo kati yao kama katika Sinai,
Katika patakatifu.
18 # Amu 5:12; Zab 78:60; Mdo 1:9; 2:4; Efe 4:8; 1 Tim 1:13 Wewe umepaa juu, umeteka mateka,
Umepewa vipawa katikati ya wanadamu;
Naam, hata na wakaidi, BWANA Mungu akae nao.
19Na ahimidiwe Bwana,
Siku kwa siku hutuchukulia mzigo wetu;
Mungu ndiye wokovu wetu.
20 # Kum 32:39 Mungu wetu ni Mungu wa kuokoa;
Na njia za kutoka mautini zina YEHOVA Bwana.
21Naam, Mungu atakipasua kichwa cha adui zake,
Utosi wenye nywele wa mtu afululizaye kukosa.
22Bwana alisema, Kutoka Bashani nitawarudisha,
Nitawarudisha kutoka vilindi vya bahari;
23Uuchovye mguu wako katika damu ya adui zako,
Na ulimi wa mbwa zako upate sehemu yake.
24Ee Mungu, wameiona miendo yako;
Miendo ya Mungu wangu, Mfalme wangu, katika patakatifu.
25Waimbaji hutangulia, nyuma yao wapigao vinanda,
Kati ya wanawali wapiga matari.
26Mhimidini Mungu katika mikutano,
Bwana katika makusanyiko ya Israeli.
27Yuko Benyamini mdogo, mtawala wao;
Wakuu wa Yuda, kundi lao;
Wakuu wa Zabuloni;
Wakuu wa Naftali.
28Ee Mungu, uziamuru nguvu zako;
Ee Mungu, uwe hodari uliyetufanyia makuu.
29 # 2 Nya 32:23; Isa 60:16 Kwa ajili ya hekalu lako Yerusalemu
Wafalme watakuletea hedaya.
30Mkemee mnyama wa mafunjoni;
Kundi la mafahali, na ndama za watu;
Hata wanyenyekee na kuleta vipande vya fedha,
Uwatawanye watu wapendao vita.
31 # Isa 19:19; 45:14; Sef 3:10; Mdo 8:27,28 Masheki watakuja kutoka Misri,
Kushi itahimiza kumnyoshea Mungu mikono yake.
32Enyi falme za dunia, mwimbieni Mungu,
Msifuni Bwana kwa nyimbo.
33Apandaye mbingu za mbingu za tangu milele;
Aitoa sauti yake, sauti ya nguvu.
34Mhesabieni Mungu nguvu;
Enzi yake imo juu ya Israeli;
Na nguvu zake ziko mawinguni.
35 # Isa 41:10; Zek 10:12; Yn 15:5; Efe 6:10; Flp 4:13 Mungu ni mwenye kutisha
Kutoka patakatifu pako.
Ndiye Mungu wa Israeli;
Yeye huwapa watu wake nguvu na uwezo.
Na ahimidiwe Mungu.

Iliyochaguliwa sasa

Zaburi 68: SRUV

Kuonyesha

Shirikisha

Nakili

None

Je, ungependa vivutio vyako vihifadhiwe kwenye vifaa vyako vyote? Jisajili au ingia