Hesabu UTANGULIZI
UTANGULIZI
Jina la kitabu hiki, “Hesabu” latokana na Kigiriki “Arithmoi” na Kilatini “Numeri”. Kuna orodha mbalimbali za watu na hesabu au sensa mbili za Waisraeli ambazo zinatajwa katika kitabu chenyewe. Katika kitabu hiki (cha nne miongoni mwa vitabu vitano vya kwanza vya Biblia), tunaelezwa jinsi Mose alivyowahesabu Waisraeli kabla ya kuanza safari yao kutoka mlima Sinai, na tena baadaye katika nchi ya Moabu, mashariki ya mto Yordani. Kitabu hiki cha Hesabu chakamilisha na kumaliza masimulizi ya vitabu vya Kutoka na Walawi.
Kitabu chenyewe chaeleza jinsi Waisraeli baada ya kupokea maagizo yote ya Mungu kule Sinai, walisafiri jangwani kuelekea nchi ya ahadi (1:1–10:10). Kwanza waliwasili Kadeshi Barnea kusini mwa nchi hiyo, lakini hawakufaulu kuingia. Hivyo ikawabidi kukaa jangwani miaka arubaini, muda ambapo walijitayarisha na mwishowe wakaichukua nchi ya Moabu mashariki mwa Bahari ya Chumvi (10:11–21:35). Sura za mwisho za kitabu hiki zinasimulia matukio yaliyohusu kutekwa kwa nchi ya Moabu; kutoka humo Waisraeli wataingia katika nchi waliyoahidiwa (22:1–36:13).
Kitabu hiki kinatupa picha ya Waisraeli katika hali yao halisi ya kibinadamu wenye matumaini na mashaka, wenye nguvu na dhaifu. Kinaonesha pia uaminifu wa Mungu katika kuwalinda watu wake.
Iliyochaguliwa sasa
Hesabu UTANGULIZI: SCLDC10
Kuonyesha
Shirikisha
Nakili
Je, ungependa vivutio vyako vihifadhiwe kwenye vifaa vyako vyote? Jisajili au ingia
Swahili Common Language DC Bible: Biblia Habari Njema kwa Watu Wote (Yenye Vitabu vya Deuterokanoni): Tafsiri ya Ushirikiano wa Makanisa (BHN): Hakimiliki © Chama cha Biblia cha Tanzania na Chama cha Biblia cha Kenya, 1995, 2001. Haki zote zimehifadhiwa.