Isaya 12
12
Wimbo wa shukrani
1Siku hiyo mtasema:
“Nakushukuru, ee Mwenyezi-Mungu,
maana ingawa ulinikasirikia,
hasira yako imetulia,
nawe umenifariji.
2 #12:2 Taz Kut 15:2; Zab 118:14 Mungu ndiye mwenye kuniokoa,
nitamtegemea yeye, wala sitaogopa;
Mwenyezi-Mungu hunijalia nguvu;
yeye mwenyewe ndiye aniokoaye.”
3Mtachota maji kwa furaha
kutoka visima vya wokovu.
4Siku hiyo mtasema:
“Mshukuruni Mwenyezi-Mungu
mwombeni kwa jina lake.
Yajulisheni mataifa matendo yake,
tangazeni kuwa jina lake limetukuka.
5Mwimbieni Mwenyezi-Mungu sifa
kwa kuwa ametenda mambo makuu;
haya na yajulikane duniani kote.
6Pazeni sauti na kuimba kwa furaha,
enyi wakazi wa Siyoni,
maana aliye mkuu miongoni mwenu
ndiye Mungu, Mtakatifu wa Israeli.”
Iliyochaguliwa sasa
Isaya 12: BHN
Kuonyesha
Shirikisha
Nakili
Je, ungependa vivutio vyako vihifadhiwe kwenye vifaa vyako vyote? Jisajili au ingia
Biblia Habari Njema kwa Watu Wote (Yenye Vitabu vya Deuterokanoni): Tafsiri ya Ushirikiano wa Makanisa (BHN): Hakimiliki -1995, 2001: kwa Chama cha Biblia cha Tanzania na Chama cha Biblia cha Kenya. Haki zote zimehifadhiwa.