Chapa ya Youversion
Ikoni ya Utafutaji

Zaburi 116

116
Shukrani kwa kuokolewa kifoni
1Nampenda Mwenyezi-Mungu,
kwa maana anisikia,
maana amesikia kilio cha ombi langu.
2Yeye amenitegea sikio,
hivyo nitamwomba muda wote niishio.
3Hatari ya kifo ilinizunguka,
vitisho vya kaburi vilinivamia;
nilijawa na mahangaiko na majonzi.
4Kisha nikamlilia Mwenyezi-Mungu:
“Ee Mwenyezi-Mungu, tafadhali unisalimishe!”
5Mwenyezi-Mungu amejaa wema na uaminifu;
Mungu wetu ni mwenye huruma.
6Mwenyezi-Mungu huwalinda wanyofu;
nilipokuwa nimekandamizwa aliniokoa.
7Uwe na utulivu mkuu, ee nafsi yangu,
maana Mwenyezi-Mungu amenitendea mema.
8Ameniokoa kifoni na kufuta machozi yangu;
akanilinda nisije nikaanguka.
9Nitatembea mbele yake Mwenyezi-Mungu,
katika nchi ya watu walio hai.
10 # Taz 2Kor 4:13 Nilikuwa na imani hata niliposema:
“Mimi nimetaabika mno.”
11Hata nilisema kwa hofu yangu:
“Binadamu wote hawaaminiki!”
12Nimrudishie nini Mwenyezi-Mungu,
kwa ukarimu wote alionitendea?
13Nitamtolea tambiko ya divai kwa kunikomboa,
nitaomba kwa jina lake Mwenyezi-Mungu.
14Nitamtimizia Mwenyezi-Mungu nadhiri zangu,
mbele ya watu wake wote.
15Kifo cha waaminifu wake Mwenyezi-Mungu
si jambo dogo mbele yake.
16Ee Mwenyezi-Mungu, mimi ni mtumishi wako;
ni mtumishi wako, mtoto wa mjakazi wako;
umenifungulia vifungo vyangu.
17Nitakutolea tambiko za shukrani,
na kukupa heshima zangu.
18Nitakutimizia ahadi zangu, ee Mwenyezi-Mungu
mbele ya watu wako wote,
19waliokusanyika hekaluni mwako,
katikati ya Yerusalemu.
Msifuni Mwenyezi-Mungu!

Iliyochaguliwa sasa

Zaburi 116: BHN

Kuonyesha

Shirikisha

Nakili

None

Je, ungependa vivutio vyako vihifadhiwe kwenye vifaa vyako vyote? Jisajili au ingia