Chapa ya Youversion
Ikoni ya Utafutaji

Zaburi 127

127
Bila Mungu kazi ya binadamu haifai
(Wimbo wa Kwenda Juu, wa Solomoni)
1Mwenyezi-Mungu asipoijenga nyumba,
waijengao wanajisumbua bure.
Mwenyezi-Mungu asipoulinda mji,
waulindao wanakesha bure.
2Mnajisumbua bure kuamka mapema asubuhi
na kuchelewa kwenda kupumzika jioni,
mjipatie chakula kwa jasho lenu.
Mungu huwaruzuku walio wake hata walalapo.
3Watoto ni riziki kutoka kwa Mwenyezi-Mungu;
watoto ni tuzo lake kwetu sisi.
4Watoto waliozaliwa wazazi wakiwa bado vijana,
ni kama mishale mikononi mwa askari.
5Heri mtu aliye na mishale hiyo kwa wingi.
Hatashindwa atakapokabiliana na adui mahakamani.

Iliyochaguliwa sasa

Zaburi 127: BHN

Kuonyesha

Shirikisha

Nakili

None

Je, ungependa vivutio vyako vihifadhiwe kwenye vifaa vyako vyote? Jisajili au ingia