Chapa ya Youversion
Ikoni ya Utafutaji

Zaburi 131

131
Kumtumainia Mungu kwa utulivu
(Wimbo wa Kwenda Juu, wa Daudi)
1Ee Mwenyezi-Mungu, sina moyo wa kiburi;
mimi si mtu wa majivuno.
Sijishughulishi na mambo makuu,
au yaliyo ya ajabu mno kwangu.
2Ila nafsi yangu imetulia na kuwa na amani,
kama mtoto mchanga alivyotulia na mama yake;
ndivyo nafsi yangu ilivyo tulivu.
3Ee Israeli, umtumainie Mwenyezi-Mungu,
tangu sasa na hata milele.

Iliyochaguliwa sasa

Zaburi 131: BHN

Kuonyesha

Shirikisha

Nakili

None

Je, ungependa vivutio vyako vihifadhiwe kwenye vifaa vyako vyote? Jisajili au ingia