Chapa ya Youversion
Ikoni ya Utafutaji

Zaburi 42

42
KITABU CHA PILI
(Zaburi 42–72)
Sala ya Mkimbizi#42-43 Zaburi 42 na 43 bila shaka zilikuwa wimbo mmoja hapo awali kama inavyoonekana dhahiri katika marudio ya aya ya 6 Zab 42 katika aya ya 11 na katika Zab 43 aya ya 5.
(Kwa Mwimbishaji. Utenzi wa Wakorahi)
1Kama paa atamanivyo maji ya kijito,
ndivyo ninavyokutamani, ee Mungu wangu!
2Naona kiu ya Mungu, kiu ya Mungu aliye hai.
Nitafika lini kwake na kuuona uso wake?
3Machozi yamekuwa chakula changu mchana na usiku,
waliponiambia kila siku: “Yuko wapi Mungu Wako!”
4Nakumbuka tena mambo haya
kwa majonzi moyoni mwangu:
Jinsi nilivyokwenda na umati wa watu,
nikawaongoza kwenda nyumbani kwa Mungu
wakipiga vigelegele vya shukrani;
umati wa watu wakifanya sherehe!
5Mbona nasononeka hivyo moyoni?
Kwa nini nahangaika hivyo ndani mwangu?
Nitamtumainia Mungu,
maana nitamsifu tena
yeye aliye msaada wangu na Mungu wangu.
6Nimesongwa na huzuni moyoni mwangu,
kwa hiyo ninakukumbuka wewe, ee Mungu,
kutoka katika eneo la Yordani,
kutoka mlima Hermoni na Mizari.
7Nimeporomoshewa mafuriko ya maji
mafuriko ya maji yaja karibu
nayo yaita maporomoko mapya.
Mawimbi na mapigo yako yamenikumba.
8Mwenyezi-Mungu atanijalia fadhili zake mchana;
nami nimwimbie wimbo wa sifa usiku,
nimwombe Mungu anipaye uhai.
9Namwambia Mungu, mwamba wangu:
“Kwa nini umenisahau?
Yanini niende huko na huko nikiomboleza
kwa kudhulumiwa na adui yangu?”
10Nimepondwa kwa matukano yao,
wanaponiuliza kila siku:
“Yuko wapi, Mungu wako!”
11Mbona nasononeka hivyo moyoni?
Kwa nini nahangaika hivyo?
Nitamtumainia Mungu,
maana nitamsifu tena Mungu,
aliye msaada wangu na Mungu wangu.

Iliyochaguliwa sasa

Zaburi 42: BHN

Kuonyesha

Shirikisha

Nakili

None

Je, ungependa vivutio vyako vihifadhiwe kwenye vifaa vyako vyote? Jisajili au ingia