Chapa ya Youversion
Ikoni ya Utafutaji

Zaburi 78:32-39

Zaburi 78:32-39 BHN

Hata hivyo waliendelea kumkosea Mungu; ijapokuwa alitenda maajabu, hawakuamini. Basi, akazikatisha siku zao kama pumzi, miaka yao kwa maafa ya ghafla. Kila alipowaua, waliobaki walimgeukia; walitubu, wakamgeukia Mungu kwa moyo. Walikumbuka kwamba Mungu alikuwa mwamba wao; Mungu Mkuu alikuwa mkombozi wao. Lakini walimdanganya kwa maneno yao; kila walichomwambia kilikuwa uongo. Hawakuambatana naye kwa moyo, hawakuwa waaminifu kwa agano lake. Lakini Mungu mwenye huruma alisamehe uovu wao, na wala hakuwaangamiza. Mara nyingi aliizuia hasira yake, wala hakuiacha ghadhabu yake yote iwake. Alikumbuka kwamba wao ni watu tu; ni kama upepo upitao na kutoweka.

Soma Zaburi 78