Chapa ya Youversion
Ikoni ya Utafutaji

Soma Biblia Kila Siku JANUARI/2023Mfano

Soma Biblia Kila Siku JANUARI/2023

SIKU 25 YA 31

Mara nyingi Wakristo wanapopoa kiroho, ibada na kazi zote za kanisani huonekana kama mzigo kwao. Ndivyo ilivyotokea kwa Israeli wakati wa Malaki. Walisahau kutoa sadaka waliyomwahidi Mungu au walimtolea kitu duni. Huku ni kumdanganya Mungu, lakini hawakuona shida, maana dhamiri zao hazikuwashtaki. Somo hutukumbusha kuwa Mungu hadanganyiki. Mtu mwenye kudanganya amelaaniwa, kwani kila mtu apandacho ndicho atakachovuna. Tutafute kuwa hai kiroho ili tumtumikie Mungu kwa moyo mweupe bila kuchoka!

siku 24siku 26

Kuhusu Mpango huu

Soma Biblia Kila Siku JANUARI/2023

Soma Biblia Kila Siku Januari/2023 ni mpango wa kusoma Biblia sehemu kwa sehemu kila siku kwa mwezi wa Januari pamoja na maelezo mafupi yatakayokusaidia kuelewa kwa urahisi na kuendelea kutafakari neno la Mungu ulilosoma kwa siku husika. Katika mpango huu utasoma zaidi katika kitabu cha Mithali, Yohana na Malaki. Karibu kujiunga na mpango huu na usome bure

More

Tungependa kuwashukuru Soma Biblia kwa kutoa mpango huu. Kwa habari zaidi, tafadhali tembelea: https://www.somabiblia.or.tz/