Soma Biblia Kila Siku 03/2025Mfano

Si halali kwako kuwa na mke wa nduguyo(m.18). Kwa maneno haya Yohana Mbatizaji alikuwa amekemea dhambi ya Mfalme Herode. Ilikuwa ni hatari kubwa, lakini Yohana alimwogopaMungukuliko wanadamu. Na kweli, Mfalme Herode alikasirika, akamfunga Yohana gerezani. Mwisho Yohana akauawa, ila Herode mwenyewe hakupenda iwe hivyo,maana Herode alimwogopa Yohana; akimjua kuwa ni mtu wa haki, mtakatifu(m.20).Fundisho: Sifa nzuri ya mtumishi wa Bwana ina nguvu kubwa katika jamii! Yesu amelifafanua namna hii:Nuru yenu na iangaze mbele ya watu, wapate kuyaona matendo yenu mema, wamtukuze Baba yenu aliye mbinguni(Mt 5:16).
Andiko
Kuhusu Mpango huu

Soma Biblia Kila Siku 03/2025 ni mpango mzuri wa kusoma Biblia kila siku sehemu kwa sehemu kwa mwezi Machi pamoja na maelezo mafupi ya kukusaidia kutafakari somo ulilosoma. Katika mpango huu utasoma zaidi kitabu cha Marko, 1 Nyakati na Isaya. Karibu kujiunga na mpango huu
More
Tungependa kumshukuru Soma Biblia kwa kutoa mpango huu. Kwa habari zaidi, tafadhali tembelea: www.somabiblia.or.tz