Chapa ya Youversion
Ikoni ya Utafutaji

Matokeo ya utafutaji

Efe 4:26 (SUV)

Mwe na hasira, ila msitende dhambi; jua lisichwe na uchungu wenu bado haujawatoka;

Yak 1:19 (SUV)

Hayo mnajua, ndugu zangu wapenzi. Basi kila mtu na awe mwepesi wa kusikia, bali si mwepesi wa kusema; wala kukasirika;

Yak 1:20 (SUV)

kwa maana hasira ya mwanadamu haiitendi haki ya Mungu.

Efe 4:31 (SUV)

Uchungu wote na ghadhabu na hasira na kelele na matukano yaondoke kwenu, pamoja na kila namna ya ubaya;

Mit 19:11 (SUV)

Busara ya mtu huiahirisha hasira yake; Nayo ni fahari yake kusamehe makosa.

Mt 5:22 (SUV)

Bali mimi nawaambieni, Kila amwoneaye ndugu yake hasira itampasa hukumu; na mtu akimfyolea ndugu yake, itampasa baraza; na mtu akimwapiza, itampasa jehanum ya moto.

Zab 37:8 (SUV)

Ukomeshe hasira, uache ghadhabu, Usikasirike, mwisho wake ni kutenda mabaya.

Mit 14:29 (SUV)

Asiye mwepesi wa hasira ana fahamu nyingi; Bali mwenye roho ya hamaki hutukuza upumbavu.

Mit 15:1 (SUV)

Jawabu la upole hugeuza hasira; Bali neno liumizalo huchochea ghadhabu.

Mhu 7:9 (SUV)

Usifanye haraka kukasirika rohoni mwako, Maana hasira hukaa kifuani mwa wapumbavu.

Mit 29:11 (SUV)

Mpumbavu hudhihirisha hasira yake yote; Bali mwenye hekima huizuia na kuituliza.

Mit 16:32 (SUV)

Asiye mwepesi wa hasira ni mwema kuliko shujaa; Na mtu aitawalaye roho yake kuliko mtu atekaye mji.

Mit 15:18 (SUV)

Mtu wa hasira huchochea ugomvi; Bali asiye mwepesi wa hasira hutuliza mashindano.

Rum 12:19 (SUV)

Wapenzi, msijilipize kisasi, bali ipisheni ghadhabu ya Mungu; maana imeandikwa, Kisasi ni juu yangu mimi; mimi nitalipa, anena Bwana.

Kol 3:8 (SUV)

Lakini sasa yawekeni mbali nanyi haya yote, hasira, na ghadhabu, na uovu, na matukano, na matusi vinywani mwenu.

Zab 76:10 (SUV)

Maana hasira ya binadamu itakusifu, Masalio ya hasira utajifunga kama mshipi.

Zab 2:12 (SUV)

Shikeni yaliyo bora , asije akafanya hasira Nanyi mkapotea njiani, Kwa kuwa hasira yake itawaka upesi; Heri wote wanaomkimbilia.

Zab 95:11 (SUV)

Nikaapa kwa hasira yangu Wasiingie rahani mwangu.

Ebr 3:11 (SUV)

Kama nilivyoapa kwa hasira yangu, Hawataingia rahani mwangu.

Zab 103:9 (SUV)

Yeye hatateta sikuzote, Wala hatashika hasira yake milele.

Sef 2:2 (SUV)

kabla haijazaa hiyo amri, kabla haijapita siku ile kama makapi, kabla haijawajilia hasira kali ya BWANA, kabla haijawajilia siku ya hasira ya BWANA.

Zab 77:9 (SUV)

Mungu amesahau fadhili zake? Amezuia kwa hasira rehema zake?

Hes 12:9 (SUV)

Hasira za BWANA zikawaka juu yao; naye akaenda zake.

Ayu 9:5 (SUV)

Aiondoaye milima, nayo haina habari, Akiipindua katika hasira zake.

Ayu 5:2 (SUV)

Kwani hasira humwua mtu mpumbavu, Nao wivu humwua mjinga.