Matokeo ya utafutaji
Eze 28:8 (SUV)
Watakushusha hata shimoni; nawe utakufa kifo chao waliouawa kati ya bahari.
Mdo 26:31 (SUV)
hata walipoondoka wakasemezana, wakisema, Mtu huyu hatendi neno linalostahili kifo wala kufungwa.
Ayu 7:15 (SUV)
Hata nafsi yangu huchagua kunyongwa, Na kuchagua kifo kuliko maumivu yangu haya.
Eze 28:10 (SUV)
Utakufa kifo cha hao wasiotahiriwa, kwa mikono ya wageni; kwa maana mimi nimenena neno hili, asema Bwana MUNGU.
Kut 10:17 (SUV)
Basi sasa, nawasihi, nisameheni dhambi yangu mara hii moja tu, mkamwombe BWANA, Mungu wenu, aniondolee kifo hiki tu.
Hes 35:32 (SUV)
Tena hamtapokea fidia kwa ajili ya huyo aliyeukimbilia mji wake wa makimbilio, apate kwenda tena kuketi katika nchi, hata kifo cha kuhani mkuu.
Hes 16:29 (SUV)
Kama watu hawa wakifa kifo cha sikuzote, kama watu wote wafavyo, au kama wakipatilizwa kwa mapatilizo ya watu wote; hapo basi BWANA hakunituma mimi.
1 Sam 22:22 (SUV)
Daudi akamwambia Abiathari, Siku ile alipokuwako Doegi, Mwedomi, nalijua yakini ya kuwa atamwambia Sauli; mimi nimewapatia watu wote wa jamaa ya baba yako kifo.
Hes 35:28 (SUV)
kwa sababu ilimpasa kukaa ndani ya mji wake wa makimbilio hata kifo chake kuhani mkuu lakini kuhani mkuu atakapokwisha kufa huyo mwuaji atarudi aende nchi ya urithi wake.
Hes 23:10 (SUV)
Ni nani awezaye kufanya idadi ya mavumbi ya Yakobo, Au kuhesabu robo ya Israeli? Na nife kifo chake mwenye haki, Na mwisho wangu uwe mfano wa mwisho wake.
Hes 35:25 (SUV)
nao mkutano utamwokoa yule aliyemwua mtu na mkono wa mwenye kutwaa kisasi cha damu; tena mkutano utamrejeza katika mji wake wa makimbilio, aliokuwa anaukimbilia; naye atakaa humo hata kifo chake kuhani mkuu, aliyepakwa mafuta kwa mafuta matakatifu.
Yos 20:6 (SUV)
Naye atakaa katika mji huo, hata hapo atakaposimama mbele ya mkutano kuhukumiwa, hata kifo chake kuhani mkuu mwenye kuwapo siku hizo; ndipo yule mwuaji atarudi, na kuuendea mji wake mwenyewe, na nyumba yake mwenyewe, hata mji huo alioutoka hapo alipokimbia.
Ufu 9:6 (SUV)
Na siku zile wanadamu watatafuta mauti, wala hawataiona kamwe. Nao watatamani kufa, nayo mauti itawakimbia.
Zab 116:15 (SUV)
Ina thamani machoni pa BWANA Mauti ya wacha Mungu wake.
Ayu 3:21 (SUV)
Ambao wangojea mauti, lakini hawayapati; Na kuyachimbulia zaidi ya kutafuta hazina iliyostirika;
1 Kor 15:26 (SUV)
Adui wa mwisho atakayebatilishwa ni mauti.
Zab 49:14 (SUV)
Kama kondoo wamewekwa kwenda kuzimu, Na mauti itawachunga; Watu wanyofu watawamiliki asubuhi; Umbo lao litachakaa, kao lao ni kuzimu.
1 Kor 15:55 (SUV)
Ku wapi, Ewe mauti, kushinda kwako? U wapi, Ewe mauti, uchungu wako?
Eze 18:32 (SUV)
Maana mimi sikufurahii kufa kwake afaye, asema Bwana MUNGU; basi ghairini, mkaishi.
Yn 12:33 (SUV)
Aliyanena hayo akionyesha ni mauti gani atakayokufa.
Mit 13:14 (SUV)
Sheria ya mwenye akili ni chemchemi ya uzima, Ili kuepukana na tanzi za mauti.
Yn 18:32 (SUV)
Ili litimie lile neno lake Yesu alilolisema, akionyesha ni mauti gani atakayokufa.
Mit 14:27 (SUV)
Kumcha BWANA ni chemchemi ya uzima, Ili kuepukana na tanzi za mauti.
Zab 55:15 (SUV)
Mauti na iwapate kwa ghafula, Na washuke kuzimu wangali hai, Maana uovu u makaoni mwao na katikati yao.
Zab 68:20 (SUV)
Mungu kwetu sisi ni Mungu wa kuokoa; Na njia za kutoka mautini zina YEHOVA Bwana.