Chapa ya Youversion
Ikoni ya Utafutaji

Matokeo ya utafutaji

Eze 28:8 (SUV)

Watakushusha hata shimoni; nawe utakufa kifo chao waliouawa kati ya bahari.

Mdo 26:31 (SUV)

hata walipoondoka wakasemezana, wakisema, Mtu huyu hatendi neno linalostahili kifo wala kufungwa.

Ayu 7:15 (SUV)

Hata nafsi yangu huchagua kunyongwa, Na kuchagua kifo kuliko maumivu yangu haya.

Eze 28:10 (SUV)

Utakufa kifo cha hao wasiotahiriwa, kwa mikono ya wageni; kwa maana mimi nimenena neno hili, asema Bwana MUNGU.

Kut 10:17 (SUV)

Basi sasa, nawasihi, nisameheni dhambi yangu mara hii moja tu, mkamwombe BWANA, Mungu wenu, aniondolee kifo hiki tu.

Hes 35:32 (SUV)

Tena hamtapokea fidia kwa ajili ya huyo aliyeukimbilia mji wake wa makimbilio, apate kwenda tena kuketi katika nchi, hata kifo cha kuhani mkuu.

Hes 16:29 (SUV)

Kama watu hawa wakifa kifo cha sikuzote, kama watu wote wafavyo, au kama wakipatilizwa kwa mapatilizo ya watu wote; hapo basi BWANA hakunituma mimi.

1 Sam 22:22 (SUV)

Daudi akamwambia Abiathari, Siku ile alipokuwako Doegi, Mwedomi, nalijua yakini ya kuwa atamwambia Sauli; mimi nimewapatia watu wote wa jamaa ya baba yako kifo.

Hes 35:28 (SUV)

kwa sababu ilimpasa kukaa ndani ya mji wake wa makimbilio hata kifo chake kuhani mkuu lakini kuhani mkuu atakapokwisha kufa huyo mwuaji atarudi aende nchi ya urithi wake.

Hes 23:10 (SUV)

Ni nani awezaye kufanya idadi ya mavumbi ya Yakobo, Au kuhesabu robo ya Israeli? Na nife kifo chake mwenye haki, Na mwisho wangu uwe mfano wa mwisho wake.

Hes 35:25 (SUV)

nao mkutano utamwokoa yule aliyemwua mtu na mkono wa mwenye kutwaa kisasi cha damu; tena mkutano utamrejeza katika mji wake wa makimbilio, aliokuwa anaukimbilia; naye atakaa humo hata kifo chake kuhani mkuu, aliyepakwa mafuta kwa mafuta matakatifu.

Yos 20:6 (SUV)

Naye atakaa katika mji huo, hata hapo atakaposimama mbele ya mkutano kuhukumiwa, hata kifo chake kuhani mkuu mwenye kuwapo siku hizo; ndipo yule mwuaji atarudi, na kuuendea mji wake mwenyewe, na nyumba yake mwenyewe, hata mji huo alioutoka hapo alipokimbia.

Ufu 9:6 (SUV)

Na siku zile wanadamu watatafuta mauti, wala hawataiona kamwe. Nao watatamani kufa, nayo mauti itawakimbia.

Zab 116:15 (SUV)

Ina thamani machoni pa BWANA Mauti ya wacha Mungu wake.

Ayu 3:21 (SUV)

Ambao wangojea mauti, lakini hawayapati; Na kuyachimbulia zaidi ya kutafuta hazina iliyostirika;

1 Kor 15:26 (SUV)

Adui wa mwisho atakayebatilishwa ni mauti.

Zab 49:14 (SUV)

Kama kondoo wamewekwa kwenda kuzimu, Na mauti itawachunga; Watu wanyofu watawamiliki asubuhi; Umbo lao litachakaa, kao lao ni kuzimu.

1 Kor 15:55 (SUV)

Ku wapi, Ewe mauti, kushinda kwako? U wapi, Ewe mauti, uchungu wako?

Eze 18:32 (SUV)

Maana mimi sikufurahii kufa kwake afaye, asema Bwana MUNGU; basi ghairini, mkaishi.

Yn 12:33 (SUV)

Aliyanena hayo akionyesha ni mauti gani atakayokufa.

Mit 13:14 (SUV)

Sheria ya mwenye akili ni chemchemi ya uzima, Ili kuepukana na tanzi za mauti.

Yn 18:32 (SUV)

Ili litimie lile neno lake Yesu alilolisema, akionyesha ni mauti gani atakayokufa.

Mit 14:27 (SUV)

Kumcha BWANA ni chemchemi ya uzima, Ili kuepukana na tanzi za mauti.

Zab 55:15 (SUV)

Mauti na iwapate kwa ghafula, Na washuke kuzimu wangali hai, Maana uovu u makaoni mwao na katikati yao.

Zab 68:20 (SUV)

Mungu kwetu sisi ni Mungu wa kuokoa; Na njia za kutoka mautini zina YEHOVA Bwana.