Matokeo ya utafutaji
Mt 6:25 (SUV)
Kwa sababu hiyo nawaambieni, Msisumbukie maisha yenu, mle nini au mnywe nini; wala miili yenu, mvae nini. Maisha je! Si zaidi ya chakula, na mwili zaidi ya mavazi?
Mit 19:10 (SUV)
Maisha ya anasa hayampasi mpumbavu; Sembuse mtumwa awatawale wakuu.
1 Sam 26:24 (SUV)
Tena, angalia, kama vile maisha yako yalivyokuwa na thamani machoni pangu, kadhalika na maisha yangu na yawe na thamani machoni pa BWANA, akaniokoe katika shida zote.
Mit 31:12 (SUV)
Humtendea mema wala si mabaya, Siku zote za maisha yake.
1 Sam 7:15 (SUV)
Naye huyo Samweli akawaamua Israeli siku zote za maisha yake.
2 Tim 3:12 (SUV)
Naam, na wote wapendao kuishi maisha ya utauwa katika Kristo Yesu wataudhiwa.
Mwa 47:8 (SUV)
Farao akamwuliza Yakobo, Je! Siku za miaka ya maisha yako ni ngapi?
Ayu 7:7 (SUV)
Kumbuka ya kwamba maisha yangu ni upepo; Jicho langu halitaona mema tena.
Lk 12:23 (SUV)
Kwa kuwa maisha ni zaidi ya chakula, na mwili ni zaidi ya mavazi.
1 Kor 15:19 (SUV)
Kama katika maisha haya tu tumemtumaini Kristo, sisi tu maskini kuliko watu wote.
Mdo 15:26 (SUV)
watu waliohatirisha maisha yao kwa ajili ya jina la Bwana wetu Yesu Kristo.
1 Kor 6:3 (SUV)
Hamjui ya kuwa mtawahukumu malaika, basi si zaidi sana mambo ya maisha haya?
Zab 128:5 (SUV)
BWANA akubariki toka Sayuni; Uone uheri wa Yerusalemu siku zote za maisha yako;
Mit 4:10 (SUV)
Mwanangu, sikiliza, na kuzipokea kauli zangu; Na miaka ya maisha yako itakuwa mingi.
Mit 9:11 (SUV)
Maana, kwa msaada wangu siku zako zitazidishwa; Na miaka ya maisha yako itaongezwa.
Ayu 11:17 (SUV)
Na maisha yako yatakuwa meupe kuliko adhuhuri; Lijapokuwa ni giza, litakuwa kama alfajiri.
1 Fal 15:6 (SUV)
Basi kulikuwa na vita kati ya Rehoboamu na Yeroboamu siku zote za maisha yake.
Mhu 6:12 (SUV)
Kwa maana ni nani ajuaye yaliyo mema ya mwanadamu katika maisha yake, siku zote za maisha yake ya ubatili, anayoishi kama kivuli? Kwa maana ni nani awezaye kumweleza mwanadamu mambo yatakayofuata baada yake chini ya jua?
Yer 52:33 (SUV)
Naye akabadili mavazi yake ya gerezani, akala chakula mbele yake daima, siku zote za maisha yake.
Mwa 25:7 (SUV)
Hizi ndizo siku za miaka ya maisha ya Ibrahimu alizoishi, miaka mia, na sabini na mitano.
2 Fal 25:29 (SUV)
naye akambadilishia mavazi yake ya gerezani, akala chakula mbele yake daima, siku zote za maisha yake.
Ayu 10:1 (SUV)
Nafsi yangu inachoka na maisha yangu; Sitajizuia na kuugua kwangu; Nitanena kwa uchungu wa roho yangu.
Zab 23:6 (SUV)
Hakika wema na fadhili zitanifuata Siku zote za maisha yangu; Nami nitakaa nyumbani mwa BWANA milele.
Mhu 9:9 (SUV)
Uishi kwa furaha pamoja na mke umpendaye, siku zote za maisha yako ya ubatili, ulizopewa chini ya jua; siku zote za ubatili wako, kwa maana huo ni sehemu yako ya maisha; na katika taabu zako ulizozitaabika chini ya jua.
Mwa 47:9 (SUV)
Yakobo akamjibu Farao, Siku za miaka ya kusafiri kwangu ni mia na thelathini; siku za miaka ya maisha yangu zimekuwa chache, tena za taabu, wala hazikufikilia siku za miaka ya maisha ya baba zangu katika siku za kusafiri kwao.