Chapa ya Youversion
Ikoni ya Utafutaji

Matokeo ya utafutaji

Flp 4:13 (SUV)

Nayaweza mambo yote katika yeye anitiaye nguvu.

2 Kor 12:9 (SUV)

Naye akaniambia, Neema yangu yakutosha; maana uweza wangu hutimilika katika udhaifu. Basi nitajisifia udhaifu wangu kwa furaha nyingi, ili uweza wa Kristo ukae juu yangu.

2 Kor 12:10 (SUV)

Kwa hiyo napendezwa na udhaifu, na ufidhuli, na misiba, na adha, na shida, kwa ajili ya Kristo. Maana niwapo dhaifu ndipo nilipo na nguvu.

Isa 40:29 (SUV)

Huwapa nguvu wazimiao, humwongezea nguvu yeye asiyekuwa na uwezo.

Isa 40:30 (SUV)

Hata vijana watazimia na kuchoka, na wanaume vijana wataanguka;

Isa 40:31 (SUV)

bali wao wamngojeao BWANA watapata nguvu mpya; watapanda juu kwa mbawa kama tai; watapiga mbio, wala hawatachoka; watakwenda kwa miguu, wala hawatazimia.

Zab 18:1 (SUV)

Wewe, BWANA, nguvu zangu, nakupenda sana;

Efe 6:10 (SUV)

Hatimaye, mzidi kuwa hodari katika Bwana na katika uweza wa nguvu zake.

Mk 12:30 (SUV)

nawe mpende Bwana Mungu wako kwa moyo wako wote, na kwa roho yako yote, na kwa akili zako zote, na kwa nguvu zako zote.

Isa 41:10 (SUV)

usiogope, kwa maana mimi ni pamoja nawe; usifadhaike, kwa maana mimi ni Mungu wako; nitakutia nguvu, naam, nitakusaidia, naam, nitakushika kwa mkono wa kuume wa haki yangu.

Kum 31:6 (SUV)

Iweni hodari na moyo wa ushujaa, msiogope wala msiwahofu; kwa maana BWANA, Mungu wako, yeye ndiye anayekwenda pamoja nawe, hatakupungukia wala kukuacha.

Zab 73:26 (SUV)

Mwili wangu na moyo wangu hupunguka, Bali Mungu ni mwamba wa moyo wangu Na sehemu yangu milele.

1 Nya 16:11 (SUV)

Mtakeni BWANA na nguvu zake; Utafuteni uso wake siku zote.

2 Sam 22:33 (SUV)

Mungu ndiye ngome yangu yenye nguvu; Naye huwaongoza wakamilifu katika njia yake.

Zab 28:7 (SUV)

BWANA ni nguvu zangu na ngao yangu. Moyo wangu umemtumaini, Nami nimesaidiwa; Basi, moyo wangu unashangilia, Na kwa wimbo wangu nitamshukuru.

Neh 8:10 (SUV)

Kisha akawaambia, Enendeni zenu, mle kilichonona, na kunywa kilicho kitamu, tena mpelekeeni sehemu yeye asiyewekewa kitu; maana siku hii ni takatifu kwa BWANA wetu; wala msihuzunike; kwa kuwa furaha ya BWANA ni nguvu zenu.

Mit 31:17 (SUV)

Hujifunga nguvu viunoni kama mshipi; Hutia mikono yake nguvu.

Hes 23:22 (SUV)

Mungu amewaleta kutoka Misri, Naye ana nguvu kama nguvu za nyati.

Zab 84:7 (SUV)

Huendelea toka nguvu hata nguvu, Huonekana Sayuni kila mmoja mbele za Mungu.

Isa 22:17 (SUV)

Tazama, BWANA atakutupa kwa nguvu, kama mtu mwenye nguvu; naam, atakuzonga-zonga.

Mit 21:22 (SUV)

Mwenye hekima huupandia mji wao wenye nguvu; Na kuziangusha nguvu za tumaini lao.

Ayu 6:12 (SUV)

Je! Nguvu zangu ni nguvu za mawe? Au mwili wangu, je! Ni shaba?

Dan 10:19 (SUV)

Akasema, Ee mtu upendwaye sana, usiogope; amani na iwe kwako, uwe na nguvu, naam, uwe na nguvu. Aliposema nami nikapata nguvu, nikasema, Ee Bwana wangu, na aseme Bwana wangu; kwa maana umenitia nguvu.

Zab 68:34 (SUV)

Mhesabieni Mungu nguvu; Enzi yake i juu ya Israeli; Na nguvu zake zi mawinguni.

Isa 5:22 (SUV)

Ole wao walio hodari kunywa kileo chenye nguvu, watu waume wenye nguvu kuchanganya vileo;