Matokeo ya utafutaji
Yn 3:16 (SUV)
Kwa maana jinsi hii Mungu aliupenda ulimwengu, hata akamtoa Mwanawe pekee, ili kila mtu amwaminiye asipotee, bali awe na uzima wa milele.
Rum 5:8 (SUV)
Bali Mungu aonyesha pendo lake yeye mwenyewe kwetu sisi, kwa kuwa Kristo alikufa kwa ajili yetu, tulipokuwa tungali wenye dhambi.
1 Kor 13:4 (SUV)
Upendo huvumilia, hufadhili; upendo hauhusudu; upendo hautakabari; haujivuni;
1 Kor 13:5 (SUV)
haukosi kuwa na adabu; hautafuti mambo yake; hauoni uchungu; hauhesabu mabaya;
1 Kor 13:6 (SUV)
haufurahii udhalimu, bali hufurahi pamoja na kweli;
1 Kor 13:7 (SUV)
huvumilia yote; huamini yote; hutumaini yote; hustahimili yote.
1 Yoh 4:7 (SUV)
Wapenzi, na mpendane; kwa kuwa pendo latoka kwa Mungu, na kila apendaye amezaliwa na Mungu, naye anamjua Mungu.
1 Yoh 4:8 (SUV)
Yeye asiyependa, hakumjua Mungu, kwa maana Mungu ni upendo.
1 Yoh 4:9 (SUV)
Katika hili pendo la Mungu lilionekana kwetu, kwamba Mungu amemtuma Mwanawe pekee ulimwenguni, ili tupate uzima kwa yeye.
1 Yoh 4:10 (SUV)
Hili ndilo pendo, si kwamba sisi tulimpenda Mungu, bali kwamba yeye alitupenda sisi, akamtuma Mwanawe kuwa kipatanisho kwa dhambi zetu.
Rum 8:38 (SUV)
Kwa maana nimekwisha kujua hakika ya kwamba, wala mauti, wala uzima, wala malaika, wala wenye mamlaka, wala yaliyopo, wala yatakayokuwapo, wala wenye uwezo,
Rum 8:39 (SUV)
wala yaliyo juu, wala yaliyo chini, wala kiumbe kinginecho chote hakitaweza kututenga na upendo wa Mungu ulio katika Kristo Yesu Bwana wetu.
1 Kor 13:13 (SUV)
Basi, sasa inadumu imani, tumaini, upendo, haya matatu; na katika hayo lililo kuu ni upendo.
2 Kor 2:8 (SUV)
Kwa hiyo nawasihi kumthibitishia upendo wenu.
Kol 1:8 (SUV)
naye alitueleza upendo wenu katika Roho.
Kol 3:14 (SUV)
Zaidi ya hayo yote jivikeni upendo, ndio kifungo cha ukamilifu.
Efe 4:2 (SUV)
kwa unyenyekevu wote na upole, kwa uvumilivu, mkichukuliana katika upendo;
2 Sam 1:26 (SUV)
Nimesikitika kwa ajili yako, Yonathani, ndugu yangu, Ulikuwa ukinipendeza sana; Upendo wako kwangu ulikuwa wa ajabu, Kupita upendo wa wanawake.
1 Kor 16:14 (SUV)
Mambo yenu yote na yatendeke katika upendo.
Wim 8:7 (SUV)
Maji mengi hayawezi kuuzimisha upendo, Wala mito haiwezi kuuzamisha; Kama mtu angetoa badala ya upendo Mali yote ya nyumbani mwake, Angedharauliwa kabisa.
Mit 27:5 (SUV)
Lawama ya wazi ni heri, Kuliko upendo uliositirika.
Zab 109:4 (SUV)
Badala ya upendo wangu wao hunishitaki, Ijapokuwa naliwaombea.
Gal 5:22 (SUV)
Lakini tunda la Roho ni upendo, furaha, amani, uvumilivu, utu wema, fadhili, uaminifu,
Efe 3:17 (SUV)
Kristo akae mioyoni mwenu kwa imani mkiwa na shina na msingi katika upendo;
Mt 24:12 (SUV)
Na kwa sababu ya kuongezeka maasi, upendo wa wengi utapoa.