Chapa ya Youversion
Ikoni ya Utafutaji

Matokeo ya utafutaji

Yn 3:16 (SUV)

Kwa maana jinsi hii Mungu aliupenda ulimwengu, hata akamtoa Mwanawe pekee, ili kila mtu amwaminiye asipotee, bali awe na uzima wa milele.

Rum 5:8 (SUV)

Bali Mungu aonyesha pendo lake yeye mwenyewe kwetu sisi, kwa kuwa Kristo alikufa kwa ajili yetu, tulipokuwa tungali wenye dhambi.

1 Kor 13:4 (SUV)

Upendo huvumilia, hufadhili; upendo hauhusudu; upendo hautakabari; haujivuni;

1 Kor 13:5 (SUV)

haukosi kuwa na adabu; hautafuti mambo yake; hauoni uchungu; hauhesabu mabaya;

1 Kor 13:6 (SUV)

haufurahii udhalimu, bali hufurahi pamoja na kweli;

1 Kor 13:7 (SUV)

huvumilia yote; huamini yote; hutumaini yote; hustahimili yote.

1 Yoh 4:7 (SUV)

Wapenzi, na mpendane; kwa kuwa pendo latoka kwa Mungu, na kila apendaye amezaliwa na Mungu, naye anamjua Mungu.

1 Yoh 4:8 (SUV)

Yeye asiyependa, hakumjua Mungu, kwa maana Mungu ni upendo.

1 Yoh 4:9 (SUV)

Katika hili pendo la Mungu lilionekana kwetu, kwamba Mungu amemtuma Mwanawe pekee ulimwenguni, ili tupate uzima kwa yeye.

1 Yoh 4:10 (SUV)

Hili ndilo pendo, si kwamba sisi tulimpenda Mungu, bali kwamba yeye alitupenda sisi, akamtuma Mwanawe kuwa kipatanisho kwa dhambi zetu.

Rum 8:38 (SUV)

Kwa maana nimekwisha kujua hakika ya kwamba, wala mauti, wala uzima, wala malaika, wala wenye mamlaka, wala yaliyopo, wala yatakayokuwapo, wala wenye uwezo,

Rum 8:39 (SUV)

wala yaliyo juu, wala yaliyo chini, wala kiumbe kinginecho chote hakitaweza kututenga na upendo wa Mungu ulio katika Kristo Yesu Bwana wetu.

1 Kor 13:13 (SUV)

Basi, sasa inadumu imani, tumaini, upendo, haya matatu; na katika hayo lililo kuu ni upendo.

2 Kor 2:8 (SUV)

Kwa hiyo nawasihi kumthibitishia upendo wenu.

Kol 1:8 (SUV)

naye alitueleza upendo wenu katika Roho.

Kol 3:14 (SUV)

Zaidi ya hayo yote jivikeni upendo, ndio kifungo cha ukamilifu.

Efe 4:2 (SUV)

kwa unyenyekevu wote na upole, kwa uvumilivu, mkichukuliana katika upendo;

2 Sam 1:26 (SUV)

Nimesikitika kwa ajili yako, Yonathani, ndugu yangu, Ulikuwa ukinipendeza sana; Upendo wako kwangu ulikuwa wa ajabu, Kupita upendo wa wanawake.

1 Kor 16:14 (SUV)

Mambo yenu yote na yatendeke katika upendo.

Wim 8:7 (SUV)

Maji mengi hayawezi kuuzimisha upendo, Wala mito haiwezi kuuzamisha; Kama mtu angetoa badala ya upendo Mali yote ya nyumbani mwake, Angedharauliwa kabisa.

Mit 27:5 (SUV)

Lawama ya wazi ni heri, Kuliko upendo uliositirika.

Zab 109:4 (SUV)

Badala ya upendo wangu wao hunishitaki, Ijapokuwa naliwaombea.

Gal 5:22 (SUV)

Lakini tunda la Roho ni upendo, furaha, amani, uvumilivu, utu wema, fadhili, uaminifu,

Efe 3:17 (SUV)

Kristo akae mioyoni mwenu kwa imani mkiwa na shina na msingi katika upendo;

Mt 24:12 (SUV)

Na kwa sababu ya kuongezeka maasi, upendo wa wengi utapoa.