Zaburi 137
137
Zaburi 137
Maombolezo ya Israeli uhamishoni
1Kando ya mito ya Babeli tuliketi, tukaomboleza
tulipokumbuka Sayuni.
2Kwenye miti ya huko
tulitundika vinubi vyetu,
3kwa maana huko hao waliotuteka
walitaka tuwaimbie nyimbo;
watesi wetu walidai nyimbo za furaha;
walisema, “Tuimbieni wimbo mmoja
kati ya nyimbo za Sayuni!”
4Tutaimbaje nyimbo za Mwenyezi Mungu,
tukiwa nchi ya kigeni?
5Nikikusahau wewe, ee Yerusalemu,
basi mkono wangu wa kuume na usahau ujuzi wake.
6Ulimi wangu ushikamane na kaakaa la kinywa changu
kama sitakukumbuka wewe,
kama nisipokufikiri Yerusalemu
kuwa furaha yangu kubwa.
7Kumbuka, Ee Mwenyezi Mungu, walichokifanya Waedomu,
siku ile Yerusalemu ilipoanguka.
Walisema, “Bomoa, bomoa
hata misingi yake!”
8Ee binti Babeli, uliyehukumiwa kuangamizwa,
heri yeye atakayekulipiza wewe
kwa yale uliyotutenda sisi:
9yeye ambaye atawakamata watoto wako wachanga
na kuwaponda juu ya miamba.
Currently Selected:
Zaburi 137: NENO
Highlight
Share
Copy
Want to have your highlights saved across all your devices? Sign up or sign in
Neno: Maandiko Matakatifu™ NMM™
Hakimiliki © 2018, 2024 na Biblica, Inc.
Imetumiwa kwa ruhusa.
Haki zote zimehifadhiwa duniani kote.
Kiswahili Contemporary Scriptures™
Copyright © 2018, 2024 by Biblica, Inc.
Used with permission. All rights reserved worldwide.