Zaburi 141
141
Zaburi 141
Maombi ya kuhifadhiwa dhidi ya uovu
Zaburi ya Daudi.
1Ee Mwenyezi Mungu, ninakuita, njoo kwangu hima.
Sikia sauti yangu ninapokuita.
2Maombi yangu na yafike mbele zako kama uvumba;
kuinua mikono yangu juu na kuwe kama dhabihu ya jioni.
3Ee Mwenyezi Mungu, weka mlinzi kinywani mwangu,
weka ulinzi mlangoni mwa midomo yangu.
4Usiuache moyo wangu uvutwe katika jambo baya,
nisije nikashiriki katika matendo maovu
pamoja na watu watendao mabaya,
wala nisije nikala vyakula vyao vya anasa.
5Mtu mwenye haki na anipige: ni jambo la huruma;
na anikemee: ni mafuta kichwani mwangu.
Kichwa changu hakitalikataa.
Hata hivyo, maombi yangu daima
ni kinyume cha watenda maovu.
6Watawala wao watatupwa chini
kutoka majabali,
waovu watajifunza kwamba maneno yangu
yalikuwa kweli.
7Watasema, “Kama mtu anavyolima na kuvunja ardhi,
ndivyo mifupa yetu imetawanywa kwenye mlango wa kaburi.”
8Lakini nimekaza macho yangu kwako, Ee Bwana Mungu Mwenyezi,
ndani yako nimekimbilia, usiniache nife.
9Niepushe na mitego waliyonitegea,
kutokana na mitego iliyotegwa na watenda maovu.
10Waovu na waanguke kwenye nyavu zao wenyewe,
wakati mimi ninapita salama.
Currently Selected:
Zaburi 141: NENO
Highlight
Share
Copy
Want to have your highlights saved across all your devices? Sign up or sign in
Neno: Maandiko Matakatifu™ NMM™
Hakimiliki © 2018, 2024 na Biblica, Inc.
Imetumiwa kwa ruhusa.
Haki zote zimehifadhiwa duniani kote.
Kiswahili Contemporary Scriptures™
Copyright © 2018, 2024 by Biblica, Inc.
Used with permission. All rights reserved worldwide.