Zaburi 140
140
Zaburi 140
Kuomba ulinzi wa Mwenyezi Mungu
Kwa mwimbishaji. Zaburi ya Daudi.
1Ee Mwenyezi Mungu, niokoe, kutoka kwa watu waovu;
nilinde na watu wenye jeuri,
2ambao hupanga mipango mibaya mioyoni mwao,
na kuchochea vita siku zote.
3Wao hufanya ndimi zao kali kama za nyoka,
sumu ya nyoka iko midomoni mwao.
4Ee Mwenyezi Mungu, niepushe na mikono ya waovu;
nilinde na watu wenye jeuri
wanaopanga kunikwaza miguu yangu.
5Wenye kiburi wameficha mtego wa kuninasa,
wametandaza kamba za wavu wao,
wametega mitego kwenye njia yangu.
6Ee Mwenyezi Mungu, ninakuambia, “Wewe ni Mungu wangu.”
Ee Mwenyezi Mungu, usikie kilio changu na kunihurumia.
7Ee Bwana Mungu Mwenyezi, Mwokozi wangu mwenye nguvu,
unikingaye kichwa changu siku ya vita:
8Ee Mwenyezi Mungu, usiwape waovu matakwa yao,
usiache mipango yao ikafanikiwa,
wasije wakajisifu.
9Vichwa vya wanaonizunguka vifunikwe na shida
zilizosababishwa na midomo yao.
10Makaa ya mawe ya moto na yawaangukie!
Na watupwe motoni,
katika mashimo ya matope,
wasiinuke tena kamwe.
11Wasingiziaji wasifanikiwe katika nchi;
maafa na yawawinde watu wenye jeuri.
12Najua kwamba Mwenyezi Mungu huwapatia maskini haki,
na kuitegemeza njia ya mhitaji.
13Hakika wenye haki watalisifu jina lako,
na waadilifu wataishi mbele zako.
Currently Selected:
Zaburi 140: NENO
Highlight
Share
Copy
Want to have your highlights saved across all your devices? Sign up or sign in
Neno: Maandiko Matakatifu™ NMM™
Hakimiliki © 2018, 2024 na Biblica, Inc.
Imetumiwa kwa ruhusa.
Haki zote zimehifadhiwa duniani kote.
Kiswahili Contemporary Scriptures™
Copyright © 2018, 2024 by Biblica, Inc.
Used with permission. All rights reserved worldwide.