1
2 Wakorintho 3:17
Neno: Maandiko Matakatifu 2024
Basi Bwana Isa ndiye Roho. Mahali alipo Roho wa Bwana Mungu Mwenyezi, hapo pana uhuru.
Linganisha
Chunguza 2 Wakorintho 3:17
2
2 Wakorintho 3:18
Nasi sote, tukiwa na nyuso zisizotiwa utaji, tunadhihirisha utukufu wa Bwana Isa kama kwenye kioo. Nasi tunabadilishwa ili tufanane naye, toka utukufu hadi utukufu mkuu zaidi, unaotoka kwa Bwana Isa, aliye Roho.
Chunguza 2 Wakorintho 3:18
3
2 Wakorintho 3:16
Lakini wakati wowote mtu anapomgeukia Bwana Mungu Mwenyezi, utaji unaondolewa.
Chunguza 2 Wakorintho 3:16
4
2 Wakorintho 3:5-6
Si kwamba sisi tunafikiri kuwa tunaweza kufanya jambo lolote wenyewe, lakini utoshelevu wetu unatoka kwa Mungu. Ndiye alitutosheleza kuwa wahudumu wa agano jipya: si wa andiko, bali wa Roho wa Mungu; kwa kuwa andiko huua, bali Roho hutia uzima.
Chunguza 2 Wakorintho 3:5-6
Nyumbani
Bibilia
Mipango
Video