Chapa ya Youversion
Ikoni ya Utafutaji

Kutoka 21:1-11

Kutoka 21:1-11 NENO

“Hizi ndizo sheria utakazoweka mbele ya Waisraeli. “Ukimnunua mtumwa Mwebrania, atakutumikia kwa miaka sita. Lakini katika mwaka wa saba, atakuwa huru naye ataenda zake pasipo kulipa chochote. Akija peke yake, ataenda huru peke yake, lakini akija na mke, ataondoka pamoja naye. Ikiwa bwana wake alimpatia mke naye akamzalia wana au binti, mwanamke pamoja na watoto wake watakuwa mali ya bwana wake, na huyo mwanaume ataondoka peke yake. “Lakini mtumishi akisema, ‘Ninampenda bwana wangu, mke wangu pamoja na watoto na sitaki kuwa huru,’ basi bwana wake atalazimika kumpeleka mbele ya waamuzi. Kisha atampeleka kwenye mlango, au kizingiti na kutoboa sikio lake kwa shazia. Naye atamtumikia bwana wake maisha yake yote. “Mtu akimuuza binti yake kuwa mtumwa, hataachwa huru kama watumwa wa kiume wanavyoachiwa. Kama hakumpendeza bwana wake aliyemchagua, huyo bwana atamwacha akombolewe. Hatakuwa na haki ya kumuuza kwa wageni, kwa sababu huyo bwana atakuwa amekosa uaminifu. Akimchagua aolewe na mwanawe, ni lazima ampe haki za kuwa binti yake. Ikiwa huyo mwana aliyeozwa mtumwa mwanamke ataoa mwanamke mwingine, ni lazima aendelee kumtosheleza huyo mke wa kwanza kwa chakula, mavazi na haki zote za ndoa. Iwapo hatamtosheleza kwa mambo hayo matatu, huyo mke wa kwanza ataondoka na kuwa huru bila malipo yoyote ya fedha.