Chapa ya Youversion
Ikoni ya Utafutaji

Kutoka 34:21-28

Kutoka 34:21-28 NENO

“Kwa siku sita utafanya kazi, lakini siku ya saba utapumzika, hata ikiwa ni majira ya kulima au ya kuvuna lazima upumzike. “Utaadhimisha Sikukuu ya Majuma kwa malimbuko ya mavuno ya ngano, na Sikukuu ya Mavuno mwishoni mwa mwaka. Mara tatu kwa mwaka wanaume wako wote watakuja mbele za Bwana Mungu Mwenyezi, Mungu wa Israeli. Nitawafukuza mataifa mbele yako na kupanua mipaka ya nchi yako, wala hakuna mtu yeyote atakayeitamani nchi yako wakati unapoenda mara tatu kila mwaka kuonana na Mwenyezi Mungu, Mungu wako. “Usinitolee damu ya dhabihu pamoja na kitu chochote chenye chachu, wala usibakize dhabihu yoyote ya Sikukuu ya Pasaka hadi asubuhi. “Leta matunda ya kwanza yaliyo bora zaidi ya ardhi yako katika nyumba ya Mwenyezi Mungu, Mungu wako. “Usimchemshe mwana-mbuzi katika maziwa ya mama yake.” Kisha Mwenyezi Mungu akamwambia Musa, “Andika maneno haya, kwa maana kulingana na maneno haya, nimefanya agano na wewe pamoja na Israeli.” Musa alikuwa huko pamoja na Mwenyezi Mungu kwa siku arobaini usiku na mchana bila kula chakula wala kunywa maji. Naye akaandika juu ya vibao maneno ya agano, yaani zile Amri Kumi.