Chapa ya Youversion
Ikoni ya Utafutaji

Mwanzo 36:1-8

Mwanzo 36:1-8 NENO

Hivi ndivyo vizazi vya Esau (yaani Edomu). Esau akaoa wake kutoka miongoni mwa wanawake wa Kanaani: Ada binti Eloni Mhiti, Oholibama binti Ana, mjukuu wa kike wa Sibeoni Mhivi; pia akaoa Basemathi binti Ishmaeli, dada yake Nebayothi. Ada akamzalia Esau Elifazi; Basemathi akamzaa Reueli; Oholibama akawazaa Yeushi, Yalamu na Kora. Hawa ndio wana wa Esau waliozaliwa kwake huko Kanaani. Esau akawachukua wake zake, watoto wake wa kiume na wa kike, na watu wote wa nyumbani mwake, mifugo yake pamoja na wanyama wake wengine wote, na mali yake yote ambayo alikuwa ameipata akiwa Kanaani, akahamia katika nchi iliyo mbali na Yakobo ndugu yake. Mali yao ilikuwa nyingi sana kiasi kwamba haikuwa rahisi wao kuishi pamoja; nchi waliyokuwa wakiishi isingewatosha wote kwa ajili ya mifugo yao. Kwa hiyo Esau (ambaye ni Edomu) aliishi katika nchi ya vilima ya Seiri.