Chapa ya Youversion
Ikoni ya Utafutaji

Zaburi 11

11
Zaburi 11
Kumtumaini Mwenyezi Mungu
Kwa mwimbishaji. Zaburi ya Daudi.
1Kwa Mwenyezi Mungu ninakimbilia.
Unawezaje basi kuniambia:
“Ruka kama ndege utorokee kwenye mlima wako.
2Hebu tazama, waovu wanapinda nyuta zao;
wanaweka mishale kwenye nyuzi zake
ili wakiwa gizani, wawapige
walio wanyofu wa moyo.
3Wakati misingi imeharibiwa,
mwenye haki anaweza kufanya nini?”
4Mwenyezi Mungu yuko ndani ya Hekalu lake takatifu;
Mwenyezi Mungu yuko kwenye kiti chake cha enzi mbinguni.
Huwaangalia wana wa watu,
macho yake yanawachunguza.
5Mwenyezi Mungu huwachunguza wenye haki,
lakini nafsi yake inachukia waovu
na wale wanaopenda mapigano.
6Atawanyeshea waovu makaa ya moto mkali
na kiberiti kinachowaka;
upepo wenye joto kali ndio fungu lao.
7Kwa kuwa Mwenyezi Mungu ni mwenye haki,
yeye hupenda haki.
Wanyofu watauona uso wake.

Iliyochaguliwa sasa

Zaburi 11: NENO

Kuonyesha

Shirikisha

Nakili

None

Je, ungependa vivutio vyako vihifadhiwe kwenye vifaa vyako vyote? Jisajili au ingia