Zaburi 13
13
Zaburi 13
Sala ya kuomba msaada
Kwa mwimbishaji. Zaburi ya Daudi.
1Hadi lini, Ee Mwenyezi Mungu? Je, utanisahau milele?
Utanificha uso wako hadi lini?
2Nitapambana na mawazo yangu hadi lini,
na kila siku kuwa na majonzi moyoni mwangu?
Adui zangu watanishinda hadi lini?
3Nitazame, unijibu, Ee Mwenyezi Mungu, Mungu wangu.
Yatie nuru macho yangu,
ama sivyo nitalala usingizi wa mauti.
4Adui yangu atasema, “Nimemshinda,”
nao adui zangu watashangilia nitakapoanguka.
5Lakini ninategemea upendo wako usiokoma;
moyo wangu unashangilia katika wokovu wako.
6Nitamwimbia Mwenyezi Mungu,
kwa kuwa amekuwa mwema kwangu.
Iliyochaguliwa sasa
Zaburi 13: NENO
Kuonyesha
Shirikisha
Nakili
![None](/_next/image?url=https%3A%2F%2Fimageproxy.youversionapistaging.com%2F58%2Fhttps%3A%2F%2Fweb-assets.youversion.com%2Fapp-icons%2Fsw.png&w=128&q=75)
Je, ungependa vivutio vyako vihifadhiwe kwenye vifaa vyako vyote? Jisajili au ingia
Neno: Maandiko Matakatifu™ NMM™
Hakimiliki © 2018, 2024 na Biblica, Inc.
Imetumiwa kwa ruhusa.
Haki zote zimehifadhiwa duniani kote.
Kiswahili Contemporary Scriptures™
Copyright © 2018, 2024 by Biblica, Inc.
Used with permission. All rights reserved worldwide.