Zaburi 36
36
Zaburi 36
Uovu wa mwanadamu
Kwa mwimbishaji. Zaburi ya Daudi mtumishi wa Mwenyezi Mungu.
1Kuna neno moyoni mwangu
kutoka kwa Mungu
kuhusu hali ya dhambi ya mwovu.
Hakuna hofu ya Mungu
mbele ya macho yake.
2Kwa kuwa machoni pake mwenyewe hujisifu mno
hata hawezi kugundua au kuichukia dhambi yake.
3Maneno ya kinywa chake ni maovu na ya udanganyifu,
ameacha kuwa mwenye hekima au kutenda mema.
4Hata kitandani mwake hupanga hila mbaya,
hujitia katika njia ya dhambi
na hakatai lililo baya.
5Upendo wako, Ee Mwenyezi Mungu, unafika hadi mbinguni,
uaminifu wako hadi kwenye anga.
6Haki yako ni kama milima mikubwa,
hukumu zako ni kama kilindi kikuu.
Ee Mwenyezi Mungu, wewe huwahifadhi
mwanadamu na mnyama.
7Upendo wako usiokoma
ni wa thamani mno!
Watu wakuu na wadogo
hujificha uvulini wa mabawa yako.
8Wanajifurahisha katika wingi ulio nyumbani mwako,
nawe utawanywesha katika mto wa furaha zako.
9Kuwa pamoja nawe ni kijito cha uzima,
katika nuru yako twaona nuru.
10Dumisha upendo wako kwa wale wanaokujua wewe,
haki yako kwa wale walio wanyofu wa moyo.
11Mguu wa mwenye kiburi usije dhidi yangu,
wala mkono wa mwovu usinifukuze.
12Tazama jinsi watenda maovu walivyoanguka:
wametupwa chini, hawawezi kuinuka!
Iliyochaguliwa sasa
Zaburi 36: NENO
Kuonyesha
Shirikisha
Nakili
Je, ungependa vivutio vyako vihifadhiwe kwenye vifaa vyako vyote? Jisajili au ingia
Neno: Maandiko Matakatifu™ NMM™
Hakimiliki © 2018, 2024 na Biblica, Inc.
Imetumiwa kwa ruhusa.
Haki zote zimehifadhiwa duniani kote.
Kiswahili Contemporary Scriptures™
Copyright © 2018, 2024 by Biblica, Inc.
Used with permission. All rights reserved worldwide.