Zab 31:1-8
Zab 31:1-8 SUV
Nimekukimbilia Wewe, BWANA, Nisiaibike milele. Kwa haki yako uniponye, Unitegee sikio lako, uniokoe hima. Uwe kwangu mwamba wa nguvu, Nyumba yenye maboma ya kuniokoa. Ndiwe genge langu na ngome yangu; Kwa ajili ya jina lako uniongoze, unichunge. Utanitoa katika wavu walionitegea kwa siri, Maana Wewe ndiwe ngome yangu. Mikononi mwako naiweka roho yangu; Umenikomboa, Ee BWANA, Mungu wa kweli. Nawachukia wao washikao yasiyofaa yenye uongo; Bali mimi namtumaini BWANA. Na nishangilie, nizifurahie fadhili zako, Kwa kuwa umeyaona mateso yangu. Umeijua nafsi yangu taabuni, Wala hukunitia mikononi mwa adui; Miguu yangu umeisimamisha panapo nafasi.