Chapa ya Youversion
Ikoni ya Utafutaji

Mithali 24:23-29

Mithali 24:23-29 SRUV

Haya nayo pia ni maneno ya wenye akili. Kupendelea watu katika hukumu si kwema. Amwambiaye mtu mwovu, Wewe una haki; Makabila ya watu watamlaani, taifa watamchukia. Bali kwao wakemeao furaha itakuwako; Na baraka ya kufanikiwa itawajilia. Aibusu midomo atoaye jawabu la haki. Tengeneza kazi yako huko nje, Jifanyizie kazi yako tayari shambani, Ukiisha, jenga nyumba yako. Usimshuhudie jirani yako pasipo sababu, Wala usidanganye kwa midomo yako. Usiseme, Nitamtenda kama alivyonitenda mimi; Nitamlipa mtu huyo sawasawa na tendo lake.

Soma Mithali 24