Chapa ya Youversion
Ikoni ya Utafutaji

Zaburi 31:1-8

Zaburi 31:1-8 SRUV

Nimekukimbilia Wewe, BWANA, Nisiaibike milele. Kwa haki yako uniponye, Unitegee sikio lako, uniokoe hima. Uwe kwangu mwamba wa nguvu, Ngome thabiti ya kuniokoa. Ndiwe mwamba wangu na ngome yangu; Kwa ajili ya jina lako uniongoze na unichunge. Utanitoa katika wavu walionitegea kwa siri, Maana Wewe ndiwe ngome yangu. Mikononi mwako naiweka roho yangu; Umenikomboa, Ee BWANA, Mungu wa kweli. Nawachukia wao washikao yasiyofaa yenye uongo; Bali mimi namtumainia BWANA. Na nishangilie, nizifurahie fadhili zako, Kwa kuwa umeyaona mateso yangu. Umeijua nafsi yangu taabuni, Wala hukunitia mikononi mwa adui; Miguu yangu umeisimamisha mahali penye usalama.

Soma Zaburi 31