Chapa ya Youversion
Ikoni ya Utafutaji

Zaburi 46:1-11

Zaburi 46:1-11 SRUV

Mungu kwetu sisi ni kimbilio na nguvu, Msaada utakaoonekana tele wakati wa mateso. Kwa hiyo hatutaogopa ijapobadilika nchi, Ijapotetemeka milima moyoni mwa bahari. Maji yake yajapovuma na kuumuka, Ijapopepesuka milima kwa kiburi chake. Kuna mto, vijito vyake vyaufurahisha mji wa Mungu, Patakatifu pa maskani zake Aliye Juu. Mungu yu katikati ya mji hautatetemeshwa; Mungu atausaidia asubuhi na mapema. Mataifa yanaghadhibika na falme kutetemeka; Anatoa sauti yake, nchi inayeyuka. BWANA wa majeshi yu pamoja nasi, Mungu wa Yakobo ni ngome yetu. Njoni muyatazame matendo ya BWANA, Jinsi alivyofanya ukiwa katika nchi. Avikomesha vita hata mwisho wa dunia; Avunja uta, akata mkuki, achoma moto magari. Tulieni, mjue ya kuwa Mimi ni Mungu, Nitakuzwa katika mataifa, nitakuzwa katika nchi. BWANA wa majeshi yu pamoja nasi, Mungu wa Yakobo ni kimbilio letu.

Soma Zaburi 46

Mipango ya Kusoma Bila Malipo na Ibada zinazohusiana na Zaburi 46:1-11