Chapa ya Youversion
Ikoni ya Utafutaji

Zaburi 13

13
Kuomba msaada
(Kwa Mwimbishaji. Zaburi ya Daudi)
1Mpaka lini ee Mwenyezi-Mungu, utanisahau?
Je, utanisahau mpaka milele?
Mpaka lini utanificha uso wako?
2Nitakuwa na wasiwasi rohoni hadi lini,
na sikitiko moyoni siku hata siku?
Hadi lini adui zangu watafurahia taabu zangu?
3Uniangalie na kunijibu, ee Mwenyezi-Mungu, Mungu wangu.
Uyaangazie macho yangu, nisipatwe na usingizi wa kifo.
4Usiwaache maadui zangu waseme: “Tumemweza huyu!”
Watesi wangu wasije wakafurahia kuanguka kwangu.
5Lakini mimi nazitumainia fadhili zako;
moyo wangu na ufurahie wokovu wako.
6Nitakuimbia wewe, ee Mwenyezi-Mungu,
kwa ukarimu mwingi ulionitendea!

Iliyochaguliwa sasa

Zaburi 13: BHN

Kuonyesha

Shirikisha

Nakili

None

Je, ungependa vivutio vyako vihifadhiwe kwenye vifaa vyako vyote? Jisajili au ingia