Chapa ya Youversion
Ikoni ya Utafutaji

Zaburi 96

96
Mungu mfalme na hakimu
(1Nya 16:23-33)
1Mwimbieni Mwenyezi-Mungu wimbo mpya!
Mwimbieni Mwenyezi-Mungu, ulimwengu wote!
2Mwimbieni Mwenyezi-Mungu na kulisifu jina lake.
Tangazeni kila siku matendo yake ya wokovu.
3Yatangazieni mataifa utukufu wake,
waambieni watu wote matendo yake ya ajabu.
4Maana Mwenyezi-Mungu ni mkuu, anasifika sana;
anastahili kuheshimiwa kuliko miungu yote.
5Miungu ya mataifa mengine si kitu;
lakini Mwenyezi-Mungu aliziumba mbingu.
6Utukufu na fahari vyamzunguka;
nguvu na uzuri vyalijaza hekalu lake.
7 # Taz Zab 29:1-2 Mpeni Mwenyezi-Mungu heshima, enyi jamii zote za watu;
naam, kirini utukufu na nguvu yake.
8Lisifuni jina lake tukufu;
leteni tambiko na kuingia hekaluni mwake.
9Mwabuduni Mwenyezi-Mungu katika patakatifu pake;#96:9 patakatifuni pake: Au Kwa mavazi ya ibada au anapotokea.
tetemekeni mbele yake ee dunia yote!
10Yaambieni mataifa: “Mwenyezi-Mungu anatawala!
Ameuweka ulimwengu imara, hautatikisika.
Atawahukumu watu kwa haki!”
11Furahini enyi mbingu na dunia!
Bahari na ivume pamoja na vyote vilivyomo!
12Furahini enyi mashamba na vyote vilivyomo!
Ndipo miti yote misituni itaimba kwa furaha,
13mbele ya Mwenyezi-Mungu anayekuja;
naam, anayekuja kuihukumu dunia.
Ataihukumu dunia kwa haki,
na mataifa kwa uaminifu wake.

Iliyochaguliwa sasa

Zaburi 96: BHN

Kuonyesha

Shirikisha

Nakili

None

Je, ungependa vivutio vyako vihifadhiwe kwenye vifaa vyako vyote? Jisajili au ingia