Chapa ya Youversion
Ikoni ya Utafutaji

Zekaria 9:9-13

Zekaria 9:9-13 BHN

Shangilieni sana enyi watu wa Siyoni! Paazeni sauti, enyi watu wa Yerusalemu! Tazama, mfalme wenu anawajieni, anakuja kwa shangwe na ushindi! Ni mpole, amepanda punda, mwanapunda, mtoto wa punda. Atatokomeza magari ya vita nchini Efraimu, na farasi wa vita kutoka mjini Yerusalemu; pinde za vita zitavunjiliwa mbali. Naye ataleta amani miongoni mwa mataifa; utawala wake utaenea toka bahari hata bahari, toka mto Eufrate hata miisho ya dunia. Mwenyezi-Mungu asema hivi: “Kwa sababu ya agano langu nanyi, agano lililothibitishwa kwa damu, nitawakomboa wafungwa wenu walio kama wamefungwa katika shimo tupu. Enyi wafungwa wenye tumaini; rudini kwenye ngome yenu. Sasa mimi ninawatangazieni: Nitawarudishieni mema maradufu. Yuda nitamtumia kama uta wangu; Efraimu nimemfanya mshale wangu. Ee Siyoni! Watu wako nitawatumia kama upanga kuwashambulia watu wa Ugiriki; watakuwa kama upanga wa shujaa.”

Soma Zekaria 9

Mipango ya Kusoma Bila Malipo na Ibada zinazohusiana na Zekaria 9:9-13