Chapa ya Youversion
Ikoni ya Utafutaji

INJILI ULIMWENGUNI - SEHEMU YA SABAMfano

INJILI ULIMWENGUNI - SEHEMU YA SABA

SIKU 6 YA 7

  

KULISHA WATU ELEFU NNE

Katika siku hizo, umati mkubwa wa watu ulikusanyika tena. Kwa kuwa walikuwa hawana chakula, Yesu akawaita wanafunzi wake akawaambia,

2 “Ninauhurumia huu umati wa watu, kwa sababu sasa wamekuwa nami kwa muda wa siku tatu na hawana chakula.Nikiwaaga waende nyumbani bila kula, watazimia njiani kwa sababu baadhi yao wametoka mbali.”

4 Wanafunzi wake wakamjibu,

“Lakini hapa nyikani tutapata wapi mikate ya kutosha kuwalisha?”

5 Yesu akawauliza,“Mna mikate mingapi?” Wakajibu, “Tuna mikate saba.”

6 Akawaambia watu waketi chini.

Akiisha kuichukua mikate saba na kushukuru, akaimega na kuwapa wanafunzi wake ili wawagawie watu.

Wanafunzi wake wakafanya hivyo.Walikuwa pia na visamaki vichache, Yesu akavibariki, akawaamuru wanafunzi wake wawagawie watu. Wale watu walikula na kutosheka,

baadaye wanafunzi wakakusanya vipande vilivyosalia wakajaza vikapu saba.Watu waliokula walikuwa wapata 4,000. Akiisha kuwaaga,

10 aliingia kwenye mashua pamoja na wanafunzi wake akaenda sehemu za Dalmanutha.

Andiko

siku 5siku 7

Kuhusu Mpango huu

INJILI ULIMWENGUNI - SEHEMU YA SABA

Mfuatano huu ni kusanyiko la hadithi kuhusu maisha Kristo itakayoshirikisha watazamaji wote ulimwenguni kwa kutumia mchanganyiko wa kuona na sauti. Maisha na mafundisho ya Yesu yalidhihirishwa katika kitabu hiki cha hadithi ambacho kinafuata masimulizi ya Agano Jipya yanayopatikana katika vitabu vya Injili vya Mathayo, Marko, Luka, na Yohana

More

Tunapenda kushukuru GNPI Afrika kwa kutoa mpango huu. Kwa habari zaidi, tafadhali tembelea: http://gnpi-africa.org