Soma Biblia Kila Siku Juni/2022Mfano
![Soma Biblia Kila Siku Juni/2022](/_next/image?url=https%3A%2F%2Fimageproxy.youversionapistaging.com%2Fhttps%3A%2F%2Fs3.amazonaws.com%2Fyvplans-staging%2F31560%2F1280x720.jpg&w=3840&q=75)
Haya, twende, tukamwue na kumtupa katika birika mojawapo, nasi tutasema, Mnyama mkali amemla; kisha tutaona zitakuwaje ndoto zake(m.20). Reubeni na Yuda hawakupenda kumwaga damu ya ndugu yao (m.21-22, 26-27). Hata hivyo hawakuzuia Yusufu kutendewa vibaya. Ila binadamu hawezi kuzuia mpango wa Mungu! Maana kwa njia ya Yusufu kufika Misri ndivyo ndoto alizopewa na Mungu zikatimizwa! Maisha yake ni mfano wa maisha ya Yesu. Yesu naye alitumwa akakataliwa; yaani,walio wake hawakumpokea(Yn 1:11).
Andiko
Kuhusu Mpango huu
![Soma Biblia Kila Siku Juni/2022](/_next/image?url=https%3A%2F%2Fimageproxy.youversionapistaging.com%2Fhttps%3A%2F%2Fs3.amazonaws.com%2Fyvplans-staging%2F31560%2F1280x720.jpg&w=3840&q=75)
Soma Biblia Kila Siku Juni/2022 ni mpango wa kusoma Biblia sehemu kwa sehemu kila siku kwa mwezi wa Juni pamoja na maelezo mafupi yatakayokusaidia kuelewa kwa urahisi na kuendelea kutafakari neno la Mungu ulilosoma kwa siku husika. Katika mpango huu utasoma zaidi katika kitabu cha Wafilipi na Mwanzo. Karibu kujiunga na mpango huu na usome bure
More
Tungependa kuwashukuru Soma Biblia kwa kutoa mpango huu. Kwa habari zaidi, tafadhali tembelea: http://www.somabblia.or.tz/