Soma Biblia Kila Siku Juni/2022Mfano
![Soma Biblia Kila Siku Juni/2022](/_next/image?url=https%3A%2F%2Fimageproxy.youversionapistaging.com%2Fhttps%3A%2F%2Fs3.amazonaws.com%2Fyvplans-staging%2F31560%2F1280x720.jpg&w=3840&q=75)
Hali ya Yusufu ikawa tena ngumu. Lakini badala ya kumlaani Mungu akazidi kumtumaini.Bwana akawa pamoja na Yusufu. Maneno haya yameandikwa mara 4 katika sura hii (m.2, 3, 21 na 23)! Na bila shaka haya yaliandikwa kutokana na masimulizi aliyosimulia Yusufu baadaye. Yaani, Yusufu aliposimulia habari hizi kwa ndugu zake na watoto wake hakujisifu bali alimpa Bwana utukufu kwa kuwa Mungualimfadhili, akampa kibali machoni pa mkuu wa gereza(m.21)! Je, unaposimulia habari ya maisha yako kwa watoto wako unampa Mungu utukufu?
Andiko
Kuhusu Mpango huu
![Soma Biblia Kila Siku Juni/2022](/_next/image?url=https%3A%2F%2Fimageproxy.youversionapistaging.com%2Fhttps%3A%2F%2Fs3.amazonaws.com%2Fyvplans-staging%2F31560%2F1280x720.jpg&w=3840&q=75)
Soma Biblia Kila Siku Juni/2022 ni mpango wa kusoma Biblia sehemu kwa sehemu kila siku kwa mwezi wa Juni pamoja na maelezo mafupi yatakayokusaidia kuelewa kwa urahisi na kuendelea kutafakari neno la Mungu ulilosoma kwa siku husika. Katika mpango huu utasoma zaidi katika kitabu cha Wafilipi na Mwanzo. Karibu kujiunga na mpango huu na usome bure
More
Tungependa kuwashukuru Soma Biblia kwa kutoa mpango huu. Kwa habari zaidi, tafadhali tembelea: http://www.somabblia.or.tz/