Chapa ya Youversion
Ikoni ya Utafutaji

Soma Biblia Kila Siku /Septemba 2023Mfano

Soma Biblia Kila Siku /Septemba 2023

SIKU 19 YA 30

Kati ya marafiki na washauri wanaotuzunguka kuna wenye nia mbaya na wengine wana lengo jema la kutusaidia. Katika kuishi na kuhusiana na hawa wote kuna haja ya kutafuta hekima ya Roho Mtakatifu ili itufundishe kupambanua ushauri wa kuupokea na ule wa kuupuuza.Mwanangu, uwe na hekima na kunifurahisha moyo wangu; ili nipate kumjibu anilaumuye(m.12). Ushauri upotoshao haufai kwako. Neno la Mungu ndilo dira yetu katika kuhusiana na wengine. Somo la leo linatufundisha umuhimu wa kujenga urafiki wa kudumu, likitukumbusha tokeo baya la kuwasahau wa nyumbani.Kama ndege aendaye huko na huko mbali na kitundu chake; Ndivyo alivyo mtu aendaye huko na huko mbali na mahali pake(m.8).

siku 18siku 20

Kuhusu Mpango huu

Soma Biblia Kila Siku /Septemba 2023

Soma Biblia Kila Siku /Septemba 2023 ni mpango mzuri wa kusoma biblia kila siku sehemu kwa sehemu kwa mwezi wa septemba pamoja na maelezo mafupi ya kukusaidia kutafakari somo ulilosoma. Katika mpango huu utasoma zaidi kitabu cha Warumi na Methali. Karibu kujiunga na mpango huu

More

Tungependa kuwashukuru Soma Biblia kwa kutoa mpango huu. Kwa habari zaidi, tafadhali tembelea: https://www.somabiblia.or.tz/