Chapa ya Youversion
Ikoni ya Utafutaji

Soma Biblia Kila Siku /Septemba 2023Mfano

Soma Biblia Kila Siku /Septemba 2023

SIKU 18 YA 30

Kujisifia ya kesho ni upumbavu, maana hatujui maisha yetu yatakavyokuwa kesho. Ni kama ukungu unaotokea kwa muda mfupi tu na kutoweka tena. Kwa hiyo kumbuka daima kumwomba Mungu sala hii, “Mapenzi yako yatimizwe”. Rafiki wa kweli ni Kristo tu. Yeye hana upendeleo. Anatuambia hali yetu yote. Neno lake linatuonya, linatuita tutubu, linatupa mwongozo na kututembeza katika maisha ya shida na ya raha. Usimwache rafiki huyu asiye mnafiki ambaye ni Kristo.

siku 17siku 19

Kuhusu Mpango huu

Soma Biblia Kila Siku /Septemba 2023

Soma Biblia Kila Siku /Septemba 2023 ni mpango mzuri wa kusoma biblia kila siku sehemu kwa sehemu kwa mwezi wa septemba pamoja na maelezo mafupi ya kukusaidia kutafakari somo ulilosoma. Katika mpango huu utasoma zaidi kitabu cha Warumi na Methali. Karibu kujiunga na mpango huu

More

Tungependa kuwashukuru Soma Biblia kwa kutoa mpango huu. Kwa habari zaidi, tafadhali tembelea: https://www.somabiblia.or.tz/